Nisamehe:Mvamizi wa Ikulu amwomba msamaha Rais Kenyatta

Mwanafunzi   wa chuo kikuu aliyejaribu kuingia ikulu  akiwa amejihami kwa kisu  Brian Kibet  amemwomba radhi rais Uhuru Kenyatta baada ya kufikishwa katika mahakama moja hapa jijini hivi leo . mashtaka dhidi yake hayakusomwa kwa sababu ripoti ya hali yake ya kiakili  iliyofanywa na hospitali ya mathari imeonyesha kwamba   ana ugonjwa unaotatizwa akili  wa  Schizophrenia. Ugonjwa huo huathiri uwezo wa kufikiria,matatizo ya kusema na pia kuvuruga mtu kujifahamu .Kibet  alijipata matatani  juni tarehe 10 mwaka huu  alipojaribu kukwea ua la ikulu ya Nairobi  akiwa amejihami kwa kisu .

Polisi waliokuwa wakilinda eneo hilo walimpiga risasi na begani na kumjeruhi na baadaye akapelekwa katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta kwa matibabu .Kibet  ni mwanafunzi wa mwaka wa tano wa uhandisi katika chuo kikuu cha JKUAT.  Familia yake imetoa  ombi kwa mahakama kuwaruhusu polisi kumhamisha hadi katika hospitali ya rufaa ya moi huko eldoret ambako aliwahi kutibiwa .

Korti itatoa uamuzi kuhusu ombi hilo la familia yake siku ya alhamisi  lakini polisi wanataka kumzuilia katika hospitali ya Mathari hadi atakapokuwa katika hali nzuri ya kujibu mashtaka dhidi yake .