Sonko wa Redio Jambo agawa kitita cha hela Machakos

IMG_20190806_092829[1]__1565098841_55646
IMG_20190806_092829[1]__1565098841_55646
Sonko wa kituo cha Jambo leo asubuhi amewashtukiza wakaazi wa mji wa Machakos na kuchana mji mzima akitafuta mshindi wa The Phrase That Pays. Sonko alianzia juhudi hizi za mchwa katika uwanja wa kuegeshea magari, Katoloni, Eastleigh na baadae kuzamia soko la kuuza mboga mjini Machakos

Soma hapa:

Mshindi wa kwanza wa shilingi elfu 5 alikuwa Kennedy Kavulunze. Washindi wengine wakiwa Leakey Mwendwa, Dominic Mumo,Susan Wanjiru,Damaris Ngina, Daniel Musyoka,Bridgid Nthoki miongoni mwa wengine.

Tazama picha za baadhi ya washindi:

Hapo kesho sonko huyu atazamia mji wa Wote ulioko kaunti ya Makueni. Sonko wa masonko atatembea viunga vya mji huu kwa udi na uvumba kumsaka atakayeng'amua The Phrase that Pays ambayo ni Redio Jambo Ongea Usikike.

Pata uhondo hapa:

Baadaye sonko wa masonko atazamia Makindu, Kibwezi na kuifunga ziara kubwa ya maeneo ya Ukambani.