Ilikuaje? Evans Otieno aelezea jinsi alivyonusurika kupatana mauti Mtaani Dandora

Evans Otieno ni mkaazi wa eneo la Dandora, amelewa na kukulia katika mtaa huo unalotambulika kama mojawapo ya maeneo hatari hapa mjini Nairobi kufuatia uwepo wa majambazi wengi.Evans alikuwa mwizi wa simu, vibeti vya wanawake na hata kuvunja majumba ya majirani wake mtaani Dandora tangu akiwa darasa la saba.

"Mimi ni mtoto wa pili kwa familia ya watoto watatu. Wazazi wangu waliaga dunia nikiwa darasa la nne hivo ikatubidi tukalewe na nyanya yetu. Hata hivyo, hali ya taanzia ilizidi kuniegemea nilipofika darasa la saba wakati nyanya yetu pia alipiga dunia teke na hivyo tukabaki watoto mayatima."

Baada ya kifo cha walezi wake, Evans alibaki bila chaguo la maisha. Kulingana na Evans pamoja na vijana wengi mtaani Dandora, Wizi tu ndio uliokuwa njia ya kipekee ya kufanikiwa maishani hapa mjini Nairobi.

"Baada ya kifo cha wazazi nilibaki bila chaguo na ndipo nilijitosa katika shughuli nzima ya wizi. Nikiwa mtoto tulikuwa tunaona majambazi wakiwa na maisha mazuri pamoja na kuwa na wapenzi warembo kweli kweli. Kwangu mimi wakati huo nilikuwa naamini kuwa ili niweze kufanikiwa lazima niwe jambazi."

 Evans aliingizwa katika shughuli hii nzima na rafikiye huku tabia na mwenendo huo ukizidi kukua kwa hali ya juu maishani mwake. La kushangaza ni kwamba, Evans pamoja na wenzake hawakuwa na uoga wowote wakati wowote wakifanya wizi wao kwani waliichukuliwa kama kazi ya kawaida tu na hivyo walikuwa wanajiamini kazini mwao.

Hata hivyo, Ili Evans aachane na tabia ya wizi aliponea chupuchupu kupatana na mauti yake.

"Niliponea mara mbili kuangamizwa. Siku moja nilimwimbia mtu simu kisha akapiga nduru. Umati wa watu ulijaa eneo hilo na wakaanza kunipiga kwa mawe. Kabla hawajaniua, Polisi waliwasili eneo hilo na wakaninusuru kwa kunitia Pingu. Mara ya pili ilikuwa tarehe 24 mwezi disemba ambapo tulikuwa na marafikizangu watatu tukifanya uhalifu. Baada ya kuimba mali ya mtu binafsi kumbe wananchi walikuwa wanatufuata. Hapo nikaambia marafiki zangu waningoje niingie msalani."

 "Nilipotoka niliona umma wa watu ukiwapiga. Mimi niliruka wa msala kwani watu walikuwa wameanza kunigeukia na kunikimbiza. Nilipofika nyumbani, Nilishindwa na kupata usingizi nikiwaza kuhusu hatma ya masiha yangu. Jirani yangu,Charles Gachaga alinieleza kuwa wote walikuwa maeiaga dunia na akaipa changamoto ya kuanzisha kufanya usafi hapo nyumbani kwangu badala ya kufanya wizi."

Kifo cha marafiki zake kilimshtua sana jambo lililobadilisha maisha yake. Evans alianzisha shirika la kuwahamasisha vijana kuachana na wizi baada ya matukio hayo na sasa shirika hilo linafanya kweli mtaani Dandora.

"Kwa sasa niliachana na wizi na kazi yangu ni kuhamasisha vijana waachane na wizi.Iwapo mtu anakataa kutusikiliza basi sisi tunamwacha pamoja na kueleza askari ili waweze kuendele ana yeye sasa kutoka hapo."

Evans amemalizia kwa kuwapa vijana wadogo pamoja na wakenya wote ushauri anao amini kuwa utawasaidia watu wote."

"Vijana mjue kua wizi hauna faida kwa utajipata mahali kuwili pekee, Jela ama Kaburini na kabla haya yatokee si jamani ubadilike kwa sababu lipo jambo unaloweza kufanyia jamii. Wakenya nanyi mjihadhari na muache tabia ya kuweka simu zenu vibetini hasa wanawake kwani hilo huwa jambo rahisi kwa jambazi kukupokonya sim yako. Kwa kulinda majumba yenu,Mwombeni mwenyezi Mungu awasaidie ila nayi mnunue kufuli za maana."