Mkusanyiko wa Habari na Matukio Muhimu 27th Novemba

 Mahakama ya leba leo imeamuru kwamba  Wilson Sossion anaweza kushikilia nyadhifa mbili ,kama katibu mkuu wa muungano wa walimu Knut na kama mbunge maalum . jaji Maureen Onyango ameamuru kwamba hakuna kinachokiuka katiba  kwa session kushikilia nyadhfa hizo mbili .wanaopinga Sossion kufanya kazi zote mbili walitaka aondolewe  KNUT kwa sababu ya kazi yake kama mbunge

 Muungano wa wauguzi umeukataa mswada wa punguza mizigo  ukisema haushughulikii mahitaji ya wauguzi .katibu mkuu Sethn Panyako  amesema  kiongozi wa Tirdway Alliance anautumia mswada huo kuendeleza  ajenda zake kisiasa .

Afisa mkuu mtendaji wa IPOA aliyefutwa kazi  Maina Njoroge amerejeshwa kazini . mwenyekiti wa maamlaka hiyo Anne Makori  amesema mkuu wa sheria  alitilia doa uamuzi wa kumfuta kazi  Maina aliyetofautiana na bodi ya maamlaka hiyo.

 Rais Uhuru  Kenyatta ametoa msaada wa shilingi milioni 2 kwa wazazi wa shule ya precious talent baada ya mkasa uliosababisha vifo vya wanafunzi wanane . kiongozi wa ODM Raila odinga naye ametoa shilingi milioni 1  akisema    silingi milioni moja ni za kuwafariji wazazi walioafiwa ilhali milioni 2 ni za kujenga shule  .

Mahakama  kuu imeamuru kwamba  picha ya  Mzee  jomo Kenyatta iliyotumiwa katika noti mpya sio ukiukaji wa katiba kwani pucha hiyo  ni sehemu ya  jumba la KICC . majaji  kanyi kimondo na Asenath Ongeri wamesema CBK haikukika sheria kwa kutumia picha hiyo katika sarafu mpya .

Serikali imeifunga shule ya msingi ya Green field  huko changamwe kwa sababu majengo yake sio salama . waziri wa elimu George Magoha  pia ameagiza shule iliyo karibu ya  Umoja kuwachukua wanafunzi 445  waliokuwa wakisomea katika shule ya Greenfiled .

 Watu 15 wameorodheshwa  kuwa miongoni mwa wanaozingatiwa kwa nafasi iliyo wazi ya  mratibu mkuu wa bajeti .mionngoni mwao ni wanawake sita  ili kuichukua nafasi hiyo iliyoachwa wazi na Agnes Odhiambo ambaye hatamu yake ilitamatika  mwishoni mwa mwaka huu  mahojiano yataanza  tarehe 9 mwezi ujao .

Maafisa wote  75,000 wa polisi watakuwa na sare mpya za samawati kufikia mwaka wa 2021 .katibu wa kudumu wa usalama wa ndani karanja Kibicho  amesema sare elfu 16  tayari zimetengezwa huku nyingine elfu 20 zikitarajiwa kuwa tayari kufikia mwisho w amwaka huu wa kifedha .

Mmiliki wa shule ya  Precious Talent Moses Ndirangu  atasalia rumande kwa siku 15 ili kuwaruhusu polisi kukamilisha uchunguzi .  mahakama ya kibera pia imewaagiza polisi kupata ripoti kutoka wizara ya elimu na idara ya mipango ya jiji ili kuwasaidia katika uchunguzi wao .

Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 7 wa gredi ya pili  ametoa hotuba  yenye hisia za simaniz kuwakumbuka wenzake walioaga dunia baada ya kuporomoka kwa jengo la madarasa ya shule ya msingi ya precipus talent . wengi waliohudhuria misa ya wafu ya wanafunzi wanane walioaga dunia katika mkasa huo walishindwa kujizuia kububujikwa machozi wakati  Abilash Muthoni alipokuwa akitoa hotuba yake .