Nilizaliwa nikiwa mpenzi wa jinsia moja, Padri wa miaka 91 asema

padri
padri

"Nilizaliwa nikiwa mpenzi wa jinsia moja. Wala sikuchagua kuwa hivi. Nimekuwa nikiishi maisha yangu yangu yote nikitamani kama ningezaliwa kuwa mtu anayeshiriki mapenzi ya mke na mume," amesema Padri Stanley Underhill.

Alipokuwa Padri wa kanisa la Anglican wakati akiwa kijana mdogo, aligundua kwamba yuko tofauti na vijana wengine. Lakini hakuwa na mtu yeyote ambaye angemueleza hisia zake.

"Sikuwahi kumwambia kaka yangu kwamba mimi ni mpenzi wa jinsia moja hadi nilipoandika kitabu changu mwaka 2018," Padri Stanley Underhill ameiambia BBC katika mahojiano na Emily Webb katika kipindi cha Outlook.

Amesema ukweli akiwa na umri wa miaka 91 na kumuarifu kaka yake ambaye ana miaka miwili chini yake.

"Hakushutuka wala kukusarikia," Underhill ameongeza. "Natamani kama ningemwambia mapema pamoja na familia yangu, lakini sikujua vile ambavyo wangechukulia uamuzi wangu."

"Nilikua katika dunia ya uhasama, ubaguzi na yenye puuza mambo pamoja na chuki, umaskini na yenye kugawanyana kimatabaka tofauti tofauti," ameandika kwa kujutia katika tawasifu wake.

Katika maisha yake, ameishi akijitahidi kuonekana kwamba yeye anashiriki mapenzi ya mume na mke.

1918 - miaka 9 kabla ya yeye kuzaliwa - wanawake walikuwa wamepata haki ya kupiga kura Uingereza, lakini kuwa mpenzi wa jinsia moja kulikuwa kukichukuliwa na wengi kama 'Chukizo kubwa machoni pa Mungu'.

Na matokeo yake, kama watu wengine ambao ni wapenzi wa jinsia moja, Underhill alificha ukweli kuhusu hali yake.

"Nilikuwa sitaki kukubali ukweli na nilichofanya ni kujikandamiza na kukana hali yangu- mimi mwenyewe, kwa wengine na hata kwa Mungu."

Aliwa mtoto, Underhill alikuwa mtu ambaye ni mwenye aibu na wazazi wake hawakuzungumzia wazi maswala ya ngono na kutengeneza mazingira magumu sana ya kuzungumzia mapenzi ya jinsia moja.

Soma zaidi