Hakuna pesa! Lusaka aahirisha vikao maalum vya kujadili ugavi wa pesa kwa kaunti

Lusaka
Lusaka
Maseneta walimfokea spika wa senate Ken Lusaka  baada ya Lusaka kuahirisha kikao maalum kilichofaa kujadili mfumo utakaotumiwa kugawa pesa kwa kaunti zote 47 .

Ni mara ya nne kwa spika kuahirisha mjadala kuhusu suala hilo   baada ya kundi aliloliteua kupata mwafaka kukosa  kukubaliana .

Kila kambi imekuwa  na msimamo mkali na kuzuia uwezekano wa kuafikia  mfumo wa pamoja unaoweza kutumiwa kugawa raslimali kwa kaunti  kwani wale ambao kaunti zao zingepata mgao wa juu wameutetea vikali mfumo mpya ilhali  wale kutoka kaunti zilizotengwa wanataka hali ya sasa isalie .

Chini ya mfumo uliopendekezwa  kaunti za  Garissa, Wajir, Marsabit, Isiolo, Samburu, Turkana, Tana River, West Pokot, Lamu  na  Mandera  zitapokea jumla  ya shilingi bilioniu 17 .

Wajir  itapoteza  shilingi bilioni 2  billion, Marsabit  na Mandera  bilioni 1.9  kila moja ilhali  Garissa  itasalimisha  shilingi bilioni  1.6 billion  nayo Tana River  itapoteza Sh1.5 billion.

Uasin Gishu, Nakuru, Kiambu, Nandi  na Kakamega c zitapata mgao wa juu .