Uamuzi kuhusu shule kufunguliwa utatolewa wiki ijayo-Magoha

magoha 3
magoha 3
Waziri wa elimu George Magoha  amesema uamuzi kuhusu ni lini shule zitafunguliwa utatolewa tarehe 25 septemba au kabla ya siku hiyo .

Magoha  ameyasema hayo jumatatu  katika mkutano na wadau wa sekta ya elimu ili kujadili  mwongozo wa kuzifungua shule katika tasasisi ya ustawishaji wa Mtaala.

Mwezi julai wizara ya elimu ilitangaza kwamba shule zitafunguliwa januri mwaka ujao . Magoha  hata hivyo alisema uamuzi  huo unaweza kubadilishwa .

Katika wiki moja iliyopita kumekuwa na shinikizo kwamba  shule zifunguliwe huku wamiliki wa shule za kibinafsi wakiitaka serikali kuzingatia uamuzi wa kutaka kuzifungua shule mwaka ujao .

Kupungua kwa visa vya maambukizi ya corona pia kumechangia wito huo wa kufunguliwa kwa  shule . Rais Uhuru Kenyatta anatarajiwa  kutoa mwongozo mpya mwishoni mwa mwezi huu   huku akilenga kufungua sekta za uchumi  ambao umevurufika tangu mwezi machi .

Shule za kibinafsi na walimu wakuu wanaitaka serikali kufungua shule mwezi ujao ili watahiniwa wa mwaka waweze kuifnya mitihani yao . Januari ilikuwa imetangazwa kama tarehe ya kufunguliwa kwa shule  iwapo visa vya  corona vingezidi lakini hali hiyo sasa imebadilika huku jumla ya visa 150 vikiripotiwa kila siku .

Hata hivyo  muungano wa walimu KNUT umekosoa mpango wa kuzifungua shule mapema  kabla ya januari .katibu mkuu Wilson Sossion  amesema shule haziko tayari kufunguliwa hata kwa watahiniwa pekee .