DP Ruto ametoa wito kwa Wakenya kuwaombea viongozi wao wakati nchi inajiandaa kwa siasa

Muhtasari
  • DP Ruto ametoa wito kwa Wakenya kuwaombea viongozi wao wakati nchi inajiandaa kwa siasa mwaka ujao
Naibu rais William Ruto akizungumza katika kanisa la House of Hope mtaani Kayole siku ya Jumapili, Januari 10, 2021.
William Ruto Naibu rais William Ruto akizungumza katika kanisa la House of Hope mtaani Kayole siku ya Jumapili, Januari 10, 2021.
Image: DPPS

Naibu Rais William Ruto ametuma ujumbe wa nia njema kwa Waislamu wote wanapoanza Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

DP katika ujumbe wake alitaka umoja wakati wa hafla ya ulimwengu.

Aliwahimiza washiriki wote kuwaombea Wakenya waendelee kuwa na amani na umoja katika nyanja zote.

 

"Kwa heshima zote, nawasihi tuwaombee watoto wetu, familia na nchi yetu ili tupate rehema za Mungu," Ruto alisema.

Alizungumza kwenye video kupitia Twitter Jumanne.

Ramadhan ni mwezi mtakatifu wa kufunga, kujitambulisha, na sala kwa Waislamu, wafuasi wa Uislamu.

Inaadhimishwa kama mwezi ambao Muhammad alipokea ufunuo wa mwanzo wa Quran, kitabu kitakatifu kwa Waislamu. Kufunga ni moja wapo ya kanuni kuu tano za Uislamu.

Hii ni mara ya pili kwa Waislamu kuashiria mwezi mtukufu tangu jangala corona lilipolipuka nchini mwaka jana Machi.

Naibu Rais William Ruto pia  ametoa wito kwa Wakenya kuwaombea viongozi wao wakati nchi inajiandaa kwa siasa mwaka ujao.