- Akisema "ameshtuka na kuchukizwa", Dkt. Matiang'i alielekeza maafisa wa usalama kuwasaka watu hao waovu na kuona wanaadhibiwa kwa vitendo vyao viovu
Waziri wa Usalama wa Ndani ametoa agizola tukio ambapo dereva wa kike alivamiwa na genge la waendesha boda boda
Akisema "ameshtuka na kuchukizwa", Dkt. Matiang'i alielekeza maafisa wa usalama kuwasaka watu hao waovu na kuona wanaadhibiwa kwa vitendo vyao viovu.
"Nimeshtushwa na kuchukizwa na video iliyosambaa ya mwendesha gari wa kike akinyanyaswa na washukiwa waendesha bodaboda kwenye barabara ya Wangari Maathai/Forest. Ni lazima tulinde barabara zetu dhidi ya vitendo hivyo viovu na vya kukemea," alisema katika taarifa yake iliyotolewa. kwenye mitandao yake ya kijamii.
Aliendelea na kusema;
"Nimewaomba maajenti wetu wa usalama kuhakikisha kwamba wahusika wote wa kitendo hiki kiovu wanakamatwa haraka na kuadhibiwa ipasavyo kwa kitendo chao hicho kiovu."
I am shocked and disgusted by a viral video clip of a female motorist being molested by suspected boda boda riders along Wangari Maathai /Forest Road.
— Dr. Fred Matiang'i (@FredMatiangi) March 7, 2022
We must protect our roads from such vile and reprehensible acts of aggression.
Huduma ya Polisi ya Kenya ilisema wanaifahamu video hiyo na kuiita "ya kuchukiza", polisi, katika taarifa iliyotumwa kwenye mitandao yao ya kijamii, walisema walitambua baadhi ya watu hao na wanawawinda.