Watoto wadogo walichomwa vibaya kutokana na shambulio la anga la Jabalia - Muuguzi wa MSF

"Watoto wadogo walifika hospitalini wakiwa na majeraha makubwa na mabaya ya moto."

Muhtasari

• "Wengi walikuwa wakipiga kelele na kuwauliza wazazi wao, nilikaa nao hadi tukapata mahali kwani hospitali ilikuwa imejaa wagonjwa."

Image: BBC

Shirika la matibabu la Médecins Sans Frontières (MSF) limeandika maelezo mafupi katika Twitter ya mmoja wa wauguzi wake wanaotoa huduma ya dharura katika hospitali ya Al Shifa katika Jiji la Gaza, ambaye aliwahudumia waathiriwa wa shambulio la anga katika kitongoji cha Jabalia.

"Watoto wadogo walifika hospitalini wakiwa na majeraha makubwa na mabaya ya moto. Walikuja bila familia zao," alisema Mohammed Hawajreh.

"Wengi walikuwa wakipiga kelele na kuwauliza wazazi wao, nilikaa nao hadi tukapata mahali kwani hospitali ilikuwa imejaa wagonjwa."

MSF ilisema ilishtushwa na shambulio la anga la Jabalia na kulaani "kipindi cha hivi punde cha vurugu zisizo na maana", huku ikitoa wito wa kusitishwa kwa mapigano."Imetosha!"

'Ripoti za kuaminika' zasema kwamba kivuko cha Rafah kinaweza kufungua kwa watu wa Gaza waliojeruhiwa

Tangu shambulio la Oktoba 7 la Hamas na jibu la kijeshi la Israel, mipaka ya Gaza imesalia kufungwa kwa kiasi kikubwa.

Lakini vyanzo mbalimbali katika eneo hilo vimependekeza mpaka wa kusini wa Rafah huenda ukafunguliwa mapema leo ili kuruhusu baadhi ya Wapalestina waliojeruhiwa vibaya kupata matibabu upande wa Misri.

Ofisi ya Mambo ya Nje ya Uingereza ilisema iliwafahamisha raia wa Uingereza waliokwama huko Gaza kuhusu kile ilichokiita ripoti za kuaminika kwamba Rafah huenda ikafunguliwa kwa ajili ya kuondoka kwa muda mfupi.

Lakini ilisema hakuna maelezo kuhusu jinsi ufunguzi huo ungesimamiwa na nani ataruhusiwa kuondoka.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani Matthew Miller alisema "hatua nzuri i" imefanywa katika mazungumzo ya kuruhusu raia wa kigeni kuondoka.

Misri imekuwa ikisita kufungua mpaka, ikihofia ongezeko lisilodhibitiwa la wakimbizi.