Mchungaji akamatwa kwa madai ya kuwalaghai wafuasi wake zaidi ya shilingi milioni 143

Bw Ebonyi alisema habari hizo ni habari "feki" zinazoenezwa na wanablogu.

Muhtasari

•Theo O Ebonyi, mashuhuri katika jimbo la Benue, anashutumiwa kwa kuwalaghai wafuasi wake na watu wengine nje ya zaidi ya shilingi 143.3milioni.

Image: BBC

Mchungaji mmoja wa Nigeria ametiwa mbaroni kwa madai ya kuwafanya watu kumuachia pesa zao kwa njia ya udanganyifu.

Theo O Ebonyi, mashuhuri katika jimbo la Benue, anashutumiwa kwa kuwalaghai wafuasi wake na watu wengine nje ya zaidi ya shilingi 143.3milioni  ($930,000; £740,000).

Alizuiliwa na kuachiliwa kwa dhamana mwaka jana, lakini hili limetolewa tu kwa umma, msemaji wa mamlaka ya kupambana na ufisadi amenukuliwa akisema.

Bw Ebonyi alisema habari hizo ni habari "feki" zinazoenezwa na wanablogu.

Hakuzungumzia tuhuma zinazomkabili.

Tume ya Uhalifu wa Kiuchumi na Kifedha ya Nigeria (EFCC) inadai Bw Ebonyi aliwataka waathiriwa wake kulipa ada ya $1,300 kila mmoja ili kupata ruzuku ya $20bn kutoka kwa Wakfu wa Ford wenye makao yake Marekani.

Walakini, inasema kwamba wakfu huo haukutoa ruzuku kama hiyo.

"Uchunguzi wa EFCC ulionyesha kuwa Ford Foundation haikuwa na mpangilio, ruzuku, uhusiano au biashara na Ebonyi,"shirika hilo lilisema katika taarifa.

"Wakfu huo ulijetenga naye pamoja na shirika moja lisilo la kiserikali ikisisitiza kuwa haina uhusiano wowote nao."

EFCC pia inadai kuwa Bw Ebonyi, ambaye anasimamia kanisa la Faith on the Rock Ministry International, alitumia pesa zilizopatikana kwa njia ya udanganyifu kununua mali yake.

Anatazamiwa kushtakiwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika, EFCC inasema. Bado haijafahamika ni mashtaka gani haswa atakabiliwa nayo.

Katika taarifa ya video ya Me Ebonyi aliyoichapisha kwenye Facebook wakati huo huo EFCC ilipotangaza kukamatwa kwake kwenye X, alisema habari za kuzuiliwa kwake zilitengenezwa na "wanablogu... kujaribu kutumia mwili wangu kupata pesa... hiyo ni habari kubwa sana ya uongo... sio kweli".

Lakini msemaji wa EFCC Dele Oyewale aliambia gazeti la Punch kwamba Bw Ebonyi alikuwa nje kwa dhamana baada ya kukamatwa na kisha kuachiliwa mwaka jana.

"Alikuwa amekamatwa kwa muda mrefu, lakini kwa sababu ya uchunguzi tuliokuwa tunafanya, hatukutoa taarifa yoyote," msemaji huyo alinukuliwa akisema.