logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Putin aongoza kura ya Urais kwa asilimia 87

Putin amekuwa akisema kila mara kuwa ana uhakika wa kuchukua kiti cha urais kwa muhula wa tano.

image
na Radio Jambo

Kimataifa18 March 2024 - 06:01

Muhtasari


•Putin amekuwa akisema kila mara kuwa ana uhakika wa kuchukua kiti cha urais kwa muhula wa tano.

Dalili za ushindi wa Vladimir Putin wa upande mmoja kama Rais wa Urusi ni dhahiri.

Wasimamizi wa uchaguzi wametangaza kuwa alipata zaidi ya asilimia 87 ya kura katika matokeo yaliyotolewa kufikia sasa.

Putin amekuwa akisema kila mara kuwa ana uhakika wa kuchukua kiti cha urais kwa muhula wa tano.

Kufuatia tangazo la maafisa wa uchaguzi, Putin alitoa maoni kwamba demokrasia ya Urusi iko wazi zaidi kuliko katika nchi nyingi za Magharibi.

Hata hivyo, hakuna kiongozi mwenye nguvu wa upinzani aliyeweza kugombea uchaguzi huo dhidi ya Putin.

Nchi za Magharibi zilishutumu uchaguzi nchini Urusi kwa kutokuwa huru na wa haki.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved