Worldcoin yafungiwa kuendesha shughuli zao Ureno, mwaka baada ya kufungiwa Kenya

Ripoti zilisema tayari zaidi ya watu 300,000 nchini Ureno walikuwa tayari wametoa data zao za kibayometriki kwa kubadilishana na malipo ya Worldcoin cryptocurrency.

Muhtasari

• Inakuja wiki tatu tu baada ya shirika la ulinzi wa data la Uhispania, AEPD, kuamuru kampuni hiyo kusimamisha shughuli zake

Mwathirika wa World Coin.
Mwathirika wa World Coin.
Image: Star, Screengrab

Mamlaka ya data ya Ureno ilitangaza Jumanne kusimamishwa kwa muda kwa mradi wa cryptocurrency Worldcoin, ikitaja wasiwasi juu ya ulinzi wa data kwa watoto katika jukwaa la skanning ya iris iliyoundwa na mtendaji mkuu wa OpenAI Sam Altman.

Worldcoin ilianza kufanya kazi mwaka jana na huwapa watumiaji kitambulisho cha kibinafsi cha kidijitali "World ID" baada ya kukaguliwa mboni ya kipekee wa iris wa macho yao.

Mradi huo, kwa mujibu wa waanzilishi wake, unalenga kutatua mojawapo ya changamoto kuu zinazokabili sekta ya crypto ambayo kwa kiasi kikubwa inategemea majina ya bandia kufanya kazi, na kuifanya iwe hatari kwa roboti za barua taka na kashfa.

Tume ya Kitaifa ya Kulinda Data ya Ureno ilihalalisha uamuzi wake, ikisema "inalinda haki ya msingi ya ulinzi wa data, hasa ya watoto," ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari.

CNPD ilisema imepokea malalamiko mengi kutoka kwa wazazi kuhusu Worldcoin kukusanya data kutoka kwa watoto wao bila ridhaa yao.

Kusimamishwa kutakuwa kwa miezi mitatu ili "kuhitimisha uchunguzi wake na kuchukua uamuzi wa mwisho," CNPD iliongeza kwa mujibu wa jarida la Hindustan.

Kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya ndani, CNPD ilisema kuwa zaidi ya watu 300,000 nchini Ureno walikuwa tayari wametoa data zao za kibayometriki kwa kubadilishana na malipo ya Worldcoin cryptocurrency.

Inakuja wiki tatu tu baada ya shirika la ulinzi wa data la Uhispania, AEPD, kuamuru kampuni hiyo kusimamisha shughuli zake baada ya kupokea malalamiko kadhaa juu ya ukusanyaji wa data kutoka kwa watoto na ukweli kwamba kuondoa kibali hairuhusiwi.