14 wafariki na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya bango kuanguka India

Huduma za dharura zinasema watu wachache bado wamenaswa chini yake na shughuli ya uokoaji inaendelea.

Muhtasari

• Serikali ya jimbo la Maharashtra, ambako Mumbai iko, imeagiza uchunguzi ufanyike kuhusu tukio hilo.

Image: REUTERS

Takriban watu 14 wameaga dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya bango kubwa kuanguka wakati wa dhoruba ya ghafla katika mji wa Mumbai nchini India.

Bango hilo, lenye ukubwa wa mita 70 kwa 50 kwa mujibu wa polisi, lilianguka kwenye nyumba na kituo cha petroli jijini siku ya Jumatatu.

Huduma za dharura zinasema watu wachache bado wamenaswa chini yake na shughuli ya uokoaji inaendelea.

Serikali ya jimbo la Maharashtra, ambako Mumbai iko, imeagiza uchunguzi ufanyike kuhusu tukio hilo.

 

Picha kwenye chaneli za habari za nchini zinaonyesha bango kubwa likiyumba kwenye upepo kabla ya kuacha njia na kuanguka kwenye majengo karibu na barabara yenye shughuli nyingi katika kitongoji cha mashariki cha jiji cha Ghatkopar. Magari kadhaa yalipondwa katika ajali hiyo.

Katika picha kutoka eneo la tukio, timu za dharura zinaweza kuonekana zikiondoa mabaki. Kanda za video zinaonyesha wafanyakazi wa uokoaji wakimtoa mwathiriwa kutoka chini ya ubao ulioanguka na kutumia zana za nguvu kukata chuma.

"Tumeokoa karibu watu 80 salama," afisa mmoja aliambia shirika la habari la ANI. "Kuna gari moja jekundu ambalo limeharibika vibaya, tunashuku kuna baadhi ya watu wamekwama ndani."