Waafrika Kusini wanapiga kura katika uchaguzi muhimu kwa ANC

Zaidi ya watu milioni 27 wamejiandikisha kupiga kura katika kura inayoangazia kuongezeka kwa mgawanyiko wa kisiasa.

Muhtasari

•Vyama 70 na wagombea huru 11 wanashiriki katika uchaguzi ambao utashuhudia Waafrika Kusini wakipigia kura bunge jipya, na mabunge tisa ya majimbo.

•Chama kikuu cha upinzani cha Democratic Alliance (DA) kimetia saini mkataba na vyama vingine 10, kukubaliana kuunda serikali ya mseto.

Image: BBC

Waafrika Kusini wanapiga kura katika uchaguzi muhimu zaidi tangu mfumo wa ubaguzi wa rangi kumalizika mwaka 1994.

Zaidi ya watu milioni 27 wamejiandikisha kupiga kura katika kura inayoangazia kuongezeka kwa mgawanyiko wa kisiasa baada ya miaka 30 ya demokrasia.

Vyama 70 na wagombea huru 11 wanashiriki katika uchaguzi ambao utashuhudia Waafrika Kusini wakipigia kura bunge jipya, na mabunge tisa ya majimbo.

"Ukuaji mkubwa wa vyama unaonyesha kukatishwa tamaa na vyama vikubwa vya zamani au, wakosoaji wanaweza kusema, watu wanatafuta fursa ya kuingia bungeni na kulipwa pensheni," mchambuzi wa kisiasa Richard Calland aliiambia BBC.

Kikiwa madarakani tangu aliyekuwa mpinga wa ubaguzi wa rangi Nelson Mandela alipoongoza kwa ushindi mwishoni mwa utawala wa wazungu wachache, chama cha African National Congress (ANC) kinawania muhula wa saba madarakani.

Ingawa ina uhakika wa "ushindi wa uhakika", kura za maoni zimekuwa zikipendekeza mara kwa mara kuwa chama hicho kitapoteza wingi wake wa wabunge kwa mara ya kwanza, na kukilazimisha kuingia katika muungano na chama kimoja au zaidi cha upinzani.

"Tunaingia katika awamu inayofuata ya demokrasia yetu, na itakuwa ni mpito mkubwa," Prof Calland aliiambia BBC.

"Tutakuwa demokrasia yenye ushindani na kukomaa zaidi, au siasa zetu zitasambaratika zaidi," aliongeza.

Kampeni hiyo imetawaliwa na ufisadi ulioenea serikalini, viwango vya juu vya ukosefu wa ajira, haswa miongoni mwa vijana, kuzorota kwa huduma za umma na uhalifu uliokithiri.

Chama kikuu cha upinzani cha Democratic Alliance (DA) kimetia saini mkataba na vyama vingine 10, kukubaliana kuunda serikali ya mseto iwapo watapata kura za kutosha kukiondoa chama cha ANC mamlakani.

Lakini hili haliwezekani sana, huku ANC ikitarajiwa kubaki chama kikubwa zaidi, na kukiweka katika nafasi nzuri ya kuongoza muungano. Ilipata 57.5% ya kura katika uchaguzi uliopita ikilinganishwa na 21% ya DA