Mtu mmoja auawa kwenye vita kuhusu mzozo wa mpaka Kisumu

Maafisa zaidi wa polisi hadi sasa wametumwa katika eneo hilo kudhibiti aina yoyote ya ongezeko zaidi.

Muhtasari
  • Mwili huo ulihamishwa hadi katika chumba kimoja cha kuhifadhia maiti cha hospitali ukingoja uchunguzi wa maiti.
Crime Scene
Image: HISANI

Mwanamume mwenye umri wa miaka 45 aliuawa kwa kukatwakatwa katika mapigano kati ya makundi mawili kuhusu mpaka huko Rabuor, Nyando kaunti ya Kisumu.

Polisi walisema wakazi wa kaunti ndogo za Kadibo na Muhoroni walikuwa wakipigana kuhusu mzozo wa mipaka.

Maafisa wa polisi na maafisa wa utawala wa serikali ya kitaifa walielekea katika eneo la tukio, ambapo walipata watu watatu kutoka kaunti ndogo ya Kadibo, walikuwa wamejeruhiwa vibaya wakati wa mapigano hayo.

Kundi la vijana zaidi ya 200 kutoka Kadibo na Muhoroni walikuwa wamekusanyika na kulaumiana kwa kuvamia ardhi ya kila mmoja.

Maafisa hao walifanikiwa kuwatuliza na waathiriwa waliojeruhiwa wote walikimbizwa katika hospitali ya kaunti ndogo ya Ahero kwa matibabu.

Otieno Karaga Koy, 45, alifariki kutokana na majeraha alipokuwa akipokea matibabu.

Mwili huo ulihamishwa hadi katika chumba kimoja cha kuhifadhia maiti cha hospitali ukingoja uchunguzi wa maiti.

Mvutano umesalia katika eneo hilo kufuatia tukio la Machi 15.

Maafisa zaidi wa polisi hadi sasa wametumwa katika eneo hilo kudhibiti aina yoyote ya ongezeko zaidi.