Ako sawa-Salasya azungumza baada ya madai Nuru Okanga amelazwa hospitali

Kulingana naye, wanamtandao wamekuwa wakimshambulia kwa kusema kuwa anampigia debe Raila ambaye hampi chochote.

Muhtasari
  • Nuru alivunja ukimya baada ya kutembelewa na Mbunge wa Mumias Mashariki Peter Salasya.
Mbunge Salasya azungumza sababu za kutonyoa nywele
Mbunge Salasya azungumza sababu za kutonyoa nywele
Image: Screengrab

Mfuasi sugu  wa Kiongozi wa Upinzani Raila Odinga Nuru Okanga amevunja ukimya baada ya ripoti kuibuka kuwa alikuwa amelazwa hospitalini baada ya kuripotiwa kukosa kuwasilisha bili ya hospitali ya takriban. Sh6000.

Nuru amevunja ukimya kwa kusema kuwa kuna baadhi ya vipengele vya watu wanaoeneza propaganda kwa lengo la kudaiwa kutumia jina lake kujipatia fedha kwa manufaa yao binafsi.

"Nilitoa mahali pesa nikalipa nikatoka ili nikiwa nje nitafute nilipe,"Okanga alisema.

Nuru alivunja ukimya baada ya kutembelewa na Mbunge wa Mumias Mashariki Peter Salasya.

Mbunge huyo kijana alimpa mwanamume huyo pesa za jumla ya Sh10,000 kwa ajili ya matumizi.

"Jeshi ako sawa, nilimtembelea kujua kama yuko hospitalini kama ilivyoripotiwa na wanablogu wajinga lakini yote ilikua propaganda. #Nuruokanga,"Aliandika Salasya.

Kupitia kwenye ujumbe wake mitandaoni Salasya alisema;

"Kimani Ichungwa baada ya kuambiwa asizungumze kuhusu Raila Odinga na Uhuru Kenyatta, sasa anaendesha uwongo kuhusu Nuru Okanga. Ilinibidi mimi binafsi niende kumuona ili nielewe kwanini wabunge wa UDA wanamsumbua sana. Serikali ndogo ikijadili kuhusu Wakenya binafsi badala ya gharama ya juu ya maisha."

Nuru Okanga tangu wakati huo ameahidi kuwa atakuwa sehemu ya waandamanaji ambao watakuwa wakiingia barabarani Jumatatu na Alhamisi bila kujali ugonjwa uliomlaza kwa siku kadhaa baada ya maandamano ya awali katika mji mkuu.

Kulingana naye, wanamtandao wamekuwa wakimshambulia kwa kusema kuwa anampigia debe Raila ambaye hampi chochote.