Kasisi wa kanisa katoliki Machakos afariki akipokea matibabu

Kabla ya kifo chake, marehemu alikuwa akifanya kazi ya kuhani msaidizi katika Parokia ya Kikatoliki ya Mbooni.

Muhtasari

• Kabla ya kifo chake, marehemu alikuwa akifanya kazi ya kuhani msaidizi katika Parokia ya Kikatoliki ya Mbooni

Kasisi Michael Musyimi Nzuki
Kasisi Michael Musyimi Nzuki
Image: Hisani

Padre Michael Musyimi Nzuki wa Jimbo Katoliki la Machakos amefariki dunia.

Kifo cha Nzuki kilitangazwa na uongozi wa Dayosisi hiyo kupitia barua ya Agosti 19, 2023.

Kulingana na barua hiyo iliyotumwa kwa makasisi wote, wanaume na wanawake wa kidini, na waumini, kasisi huyo alifariki katika hospitali ya Mater Misericordiae jijini Nairobi alikokuwa akitibiwa.

“Ni kwa masikitiko makubwa kwamba Dayosisi Katoliki ya Machakos inatangaza kifo cha Padre Michael Musyimi kilichotokea Ijumaa tarehe 17 Agosti 2023 katika Hospitali ya Mater Misericordiae. Parokia ya nyumbani kwake ni parokia ya Mavindini,” barua iliyoonekana na Star ilisomeka kwa sehemu.

Kabla ya kifo chake, marehemu alikuwa akifanya kazi ya kuhani msaidizi katika Parokia ya Kikatoliki ya Mbooni.