Hawezi kuua na kumzika mtu-Familia ya Mackenzie hatimaye yazungumza

Ndugu yake mdogo, Robert Mackenzie, akizungumza na Citizen TV anasema Paul aliacha kuhubiri 2019,

Muhtasari
  • Licha ya idadi kubwa ya miili iliyookotwa mashambani katika siku chache zilizopita, familia ya pasta inasadiki kwamba ndugu yao ndiye anayelengwa na uovu.
MCHUNGAJI PAUL MACKENZIE
Image: ALPHONSE NGARI

Familia ya mhubiri mwenye utata Paul Mackenzie imejitokeza kumtetea huku miili iliyofukuliwa ikiongezeka kila kuchao.

Ndugu yake mdogo, Robert Mackenzie, akizungumza na Citizen TV  anasema Paul aliacha kuhubiri 2019, na alianza ukulima, na kwa hivyo hahusiki na vifo vya Shakahola.

"Alianza kama opereta wa teksi huko Malindi; kazi aliyoifanya kwa miaka kadhaa kabla ya kupokea wito wake wa kiroho," Robert alisema.

Aliongeza kuwa alimuona Paul akijaribu kuhudumu katika makanisa tofauti ndani ya Malindi lakini tofauti kati yake na waanzilishi wa makanisa hayo zilionekana kuwa nyingi na hivyo kufukuzwa katika makanisa matatu.

Paul aliweza kuanzisha kanisa la Good News International (GNI).

Huduma ya mzee Mackenzie katika GNI hivi karibuni ilikua kwa idadi na katika mabishano, kupitia mafundisho yake ambayo yaliwahimiza washiriki pamoja na mambo mengine kuachana na elimu ya kisasa na kutafuta afya.

Familia yake inasema kutekeleza mafundisho hayo kamwe haikuwa lazima.

"Watoto wangu wanakwenda shule na wanaenda hospitali na Mackenzie hajawahi kunilazimisha kufanya vinginevyo," alisema Robert.

Licha ya idadi kubwa ya miili iliyookotwa mashambani katika siku chache zilizopita, familia ya pasta inasadiki kwamba ndugu yao ndiye anayelengwa na uovu.

Wanasema Paul alikuwa mtoto wa kuigwa aliyekua, mkarimu kwa kosa na asiye na uwezo wa uhalifu anaotuhumiwa sasa.

"Sikubaliani na tuhuma hizo, namfahamu kaka yangu vizuri; hakuna jinsi angeua na kumzika mtu," alisema Robert.