BBI

Tusiingize siasa katika maisha –Uhuru awaambia wanaopinga BBI

Rais awashauri wakenya kuisoma ripoti ya BBI

Muhtasari

 

  •  Rais Uhuru ameipokea Ripoti ya BBI  leo
  • Amesema wakenya wanafaa kuisoma wenyewe
Rais Uhuru Kenyatta

Rais Uhuru Kenyatta  amewakosoa wanaopinga ripti ya BBI   akisema wanafaa kuonyesha uongozi  wanaposisoma ripoti hiyo badala ya kusababisha migawanyiko .

Uhuru  amesema hatozungumza kuhusu yaliyomo katika ripoti hiyo ili watu wasimshtumu kwa kushawishi  matokeo  yake

" Hatuangalii mambo ambayo yanatugawanya . Tulete mwafaka  ili tusonge mbele .Nataka kuwaraia wanasiasa wenzangu kwamba huu sio wakati wa kuleta migawanyiko’

 Rais aliyasema hayo siku ya jumatano akipokea ripoti ya BBI   na kiongozi wa upinzani Raila Odinga   huko Kisii .

" Huu ni wakati  wa kuwaleta wakenya pamoja .Naipokea hii ripoti kwa mara ya kwanza . ndio kwa sababu tulinyamaza kuihusu  kwa ajili ya imani yetu kwenu..

 Tusiiache nafasi hii kuhariika  kwa sababu ndogo ndogo za kisiasa’

 Uhuru amesema wakenya wanafaa kuisoma ripoti hiyo kwa makini na kisha kujifanyia maamuzi .

 Rais amesema wakenya wanafaa kuisoma ripoti ya BBI  kivyao na sio kuegemea misimamo yao ya kisiasa  na kutoa maoni yao ili kuiboresha

" Leo tunaipokea ripoti hii lakini siku ya jumatatu tutapata fursa huko Bomas ili kusomewa yaliyomo hatua kwa hatua’  Uhuru amesema