- Joseph Abanta amesema wakenya ni watu wazuri na hawafai kukubali kuhadaiwa au kutumiwa vibaya na viongozi wa kisiasa
- .Mkewe alilazimika kutoka nje kwa moshi mkali uliokuwa umetanda katika nyumba yao
Mamake Pendo Lancer Achieng amesema hakuna kitakachoweza kumrejesha mtoto wake . Achieng amesema hakuna mwanamke anayefaa kuomboleza kifo cha mtoto wake , amezungumza wakati wa uzindzi wa ripoti ya BBI katika ukumbi wa Bomas
Babake mtoto Pendo ambaye aliuawa kwa kupigwa rungu na polisi wakati wa machafuko ya uchaguzi mkuu uliopita amewashauri wakenya kutohadaiwa na wanasiasa .
Joseph Abanta amesema wakenya ni watu wazuri na hawafai kukubali kuhadaiwa au kutumiwa vibaya na viongozi wa kisiasa .
‘ Acheni damu ya mtoto wangu iwe wakati wa mwisho mtu kupoteza maisha yake kwa sababu ya siasa’ amesema Abanta
Abanta amemrai rais Uhuru kutozisahau familia za waaithiriwa wa ghasia za uchaguzi wakati huu mgumu
"Naomba Rais Uhuru vile mumeshikana na Raila Odinga msiachane mkono. Naona BBI italeta mabadiliko kwa maisha yetu. Rais kumbuka familia ya Baby Pendo msituache hivo. Mumetuacha tunateseka,” amesema
Baby Pendo, aliuawa wakati polisi waliokuwa wakshika doria walipovamia nyumba yao . walikuwa wamelala mwendo wa saa sita unusu usiku waliposikia ukemi wa jirani yao aliyekuwa amevamiwa na wakaamka .
Wazazi wake Lencer Achieng na Joseph Abanja walijaribu kuzuia polisi wasiingie katika nyumba yao kwa kuweka kitanda karibu na mlango lakini walizidiwa nguvu .
Polisi baadaye walitupa kitoa machozi ndani ya nyumba yao na kufunga mlango kutoka nje .Familia hiyo ya watu wanne ilijaribu kujinasua lakini Abanja alipofaulu kutoka nje alijipata mikononi mwa polisi waliokuwa wamemngoja kwa rungu .Mkewe alilazimika kutoka nje kwa moshi mkali uliokuwa umetanda katika nyumba yao