- Visa zaidi vya corona vinaripotiwa kila siku
- wakenya wengi waepuuza kanuni za kupambana na corona
Inspekta mkuu wa polisi Hillary Mutyambai amewaonya wananchi dhidi ya kutovalia maski katika maeneo ya umma . IG amesema kupitia twitter kwamba wanaokosa kuvalia maski katika sehemu za umma watapigwa faini ya shilingi 20,000
Hata hivyo amesema polisi wanafaa kutekeleza kanuni hiyo ila wasitumie nguvu kupita kiasi .
Mutyambai pia amewataka wananchi kuripoti visa ambavyo polisi wanatumia nguvu kupindukia wakitekeleza agizo hilo kwa afisi yake IAU, au IPOA kwa hatua kuchukuliwa
1. @NPSOfficial_KE continues to enforce the MoH protocols, even tho’ this effort must be completed by all of us being responsible.
— Hillary N. Mutyambai (@IG_NPS) November 2, 2020
2. Are you willing to come to my office to substantiate these ‘FACTS’ about officers keeping records of corrupt moneys? I’ll appreciate. #EngageTheIG https://t.co/wY6nd8yvRk
Onyo hiyo yake inajiri huku rais Uhuru Kenyatta akitarajiwa kulihutubia nchi kuhusu ongezeko la visa vya corona .
Rais ameitisha mkutano na magavana ili kujadili visa vipya vya corona nchini .msemaji wa Ikulu Kanze Dena wiki jana alisema mkutano huo utafanyika tarehe nne mwezi huu .
Taifa kwa sasa imesajili visa Zaidi vya corona na vifo Zaidi ya 1000