Utalii

Baada ya kusajili hasara ya shilingi bilioni 80,sekta ya utalii inahitaji ubunifu-Balala

Sekta hiyo imeathiriw apakubw ana janga la Corona

Muhtasari

 

  •  Balala asema ubunifu sasa ndio suluhisho la kuimarisha sekta ya utalii siku zijazo
  •  Sekta ya utalii imepata hasara ya zaidi ya shilingi bilioni 80 kwa ajili ya Corona 

 

Balala
Waziri wa Utalii Najib Balala Balala

 

 Ubunifu sasa unafaa kuwa jambo la msingi kwa wadau katika sekta ya utalii ,amesema waziri wa Utalii Najib Balala .

 Katika mkutano uliofanywa kwa njia ya kidijitali siku ya jumanne Balala amesema wafanyikazi katika sekta hiyo wanafaa kupewa upya mafunzo ,kuwa wabunifu na kuvumbua mbinu mpya za kufanikisha utalii ili kusalia katika sekta hiyo .

" Huu ndio wakati wa kustahimili na kubadilisha jinsi ya kuendesha oparesheni na utoaji wa huduma katika sekta hii  ili kuifanya kuwa thabiti katika siku zijazo’ amesema

Balala  amesema sekta hiyo italazimika kutathmini  kuhusu masuala muhimu kama vile afya  na matumizi ya teknolojia pamoja na kuzihusisha jamii  kwa kuzinufaisha moja kwa moja ili kustahimili changamoto zijazo.

Kenya  imepewa muhuri wa kimataifa  wa baraza l dunia la usafiri na utalii kwa kuanzisha mikakati na  hatua za kudumisha usalama wa kiafya katika shughuli zake za kitali .

 Sekta ya utalii ni mojawapo ya zilizoathiriwa pakubwa na janga la Corona na Balala amesema mapato ya Utalii yamepungua kwa asilimia 98 na kusajili hasara ya Zaidi ya shilingi bilioni 80