- Omtatah amesema hatua hiyo ya Maraga kumteua naibu wake kutwaa majukumu yake kama jaji mkuu kuanzia disemba tarehe 12 ni ukiukaji wa sheria na katiba .
- Mwanaharakati huyo anataka mahakama kutoa agizo la muda kuzuia uamuzi wa jaji mkuu kusalimisha mamlaka yake kwa Mwilu hadi ombi lake lisikizwe.
Mwanaharakati Okiya Omtatah amewasilisha kesi nyingine kortini akitaka kumzuia naibu jaji mkuu Philomena Mwilu dhidi ya kuchukua usukani kama kaimu jaji mkuu .
Mwanaharakati huyo anapinga uamuzi wa jaji mkuu anayeondoka David Maraga kumkabidhi Mwilu madaraka yake hadi tume ya JSC itakapomteua jaji mkuu mpya .
Omtatah amesema hatua hiyo ya Maraga kumteua naibu wake kutwaa majukumu yake kama jaji mkuu kuanzia disemba tarehe 12 ni ukiukaji wa sheria na katiba .
Amesema Maraga hana maamlaka ama uwezo wa kumetua kaimu jaji mkuu kwa sababu hakuna kipengee katika katiba kinachompa maamlka ya kumteua kaimu jaji mkuu .
Bwana Omtatah pia amedai kwamba nafasi ya kaimu jaji mkuu inakiuka katiba kwani ni mtu mmoja tu anayetambuliwa kama jaji mkuu . Hata naibu jaji mkuu hufanya kazi chini ya maelekezo ya jaji mkuu
Mwanaharakati huyo anataka mahakama kutoa agizo la muda kuzuia uamuzi wa jaji mkuu kusalimisha mamlaka yake kwa Mwilu hadi ombi lake lisikizwe.