Mfanyikazi mmoja wa nyumbani ameshtakiwa kwa wizi wa shilingi laki tatu kutoka kwa mwajiri wake mtaani kileleshwa .
Consolata Luyeku amefikishwa katika mahakama ya kibera mbele ya hakimu mkuu Derrick Kuto .
Luyeku anashtumiwa kwa kuiba pesa hizo kutoka kwa Joyce Kayere katika tarehe mbali mbali kati ya oktoba 10 na 27 mwaka hiyo .
Pia alishtakiwa kwa kosa la pili la kumiliki nguo za kayere zenye thamani ya shilingi elfu 50 .
Mtuhumiwa anadaiwa kujaribu kuwasiliana nan a mlalamishi
Aliachiliwa kwa bondi ya shilingi laki tatu au dhamana ya shilingi elfu 150.
Kesi hiyo itatajwa januari tarehe 21.