BBI

Msitumie BBI kuwagawanya wakenya-Ruto

Dr Ruto aliyasema hayo siku ya jumatano wakati wa mazishi ya Nalangu Enole Ntutu, mamake seneta wa zamani wa Narok Stephen Ole Ntutu na mshirikishi wa wizara ya Leba Patrick Ole Ntutu katika boma lao Ololunga ,kaunti ya Narok

Muhtasari
  • Amewataka viongozi  kuwaruhusu wakenya kusoma na kuelewa mapendekezo yaliotolewa kuirekebisha katiba  bila kuwapa vitisho .
  •  Amesema  viongozi wanafaa kuwaelimisha wakenya kuhusu vipengee vya sheria vilivyorekebishwa  badala ya kufanya kampeni za kupinga ama kuunga mkono  kura ya maamuzi kuhusu mapendekezo hayo .

Naibu wa rais William Ruto  amewahimiza viongozi kutotumia BBI kuwagawanya wakenya .

 Amewataka viongozi  kuwaruhusu wakenya kusoma na kuelewa mapendekezo yaliotolewa kuirekebisha katiba  bila kuwapa vitisho .

 Amesema  viongozi wanafaa kuwaelimisha wakenya kuhusu vipengee vya sheria vilivyorekebishwa  badala ya kufanya kampeni za kupinga ama kuunga mkono  kura ya maamuzi kuhusu mapendekezo hayo .

“ Marekebisho ya katiba hayafai kuwagawanya wakenya na kuzua uhasama’ amesema Ruto .

Dr Ruto aliyasema hayo siku ya jumatano wakati wa mazishi ya   Nalangu Enole Ntutu, mamake seneta wa zamani wa Narok Stephen Ole Ntutu  na mshirikishi wa wizara ya Leba  Patrick Ole Ntutu katika boma lao  Ololunga  ,kaunti ya Narok

 Alikuwa ameandamana na  waziri wa Leba Simon Chelgui,  magavana Samuel Tunai (Narok), Hillary Barchok (Bomet) na  Joseph Ole Lenku (Kajiado), wabunge  Korei Ole Lemein (Narok South), Soipan Tuya (Narok) na  David Ole Sankok (Mteule ). 

 Wengine walikuwa   Johana Ng'eno (Emurua Dikirr) Ndindi Nyoro (Kiharu), Benjamin Washiali (Mumias East).