Polisi wanachunguza tukio la mauaji ya afisa wa KDF mwenye umi wa miaka 38 aliyeshambuliwa na umati wa watu siku ya krisimasi mtaani Utaweala ,Nairobi .
Aliuawa kwa kupigwa mawe na kundi moja la watu ambao alikuwa amelumbana nao akitembea kutoka baa moja .
Polisi wanasema uchunguzi wa mwanzo unaonyesha kwamba afisa huyo na kakake walikuwa wakitoka baa moja walipokutana na kundi hilo lililowashambulia .
Inadaiwa mwanajeshi huyo alimsalimua mwanamke mmoja hatua ambayo ilimhamakisha mpenzi wa mwanamke huyo na hapo ndipo ugomvi ulipozuka na baadaye kusababisha kuuawa kwa mwanajeshi huyo kwa kupigwa mawe wakati mtu na mpenzi wake walipopigwa ukemi kwamba wanashambuliwa na majambazi . Tayari watu sita wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo na watafikishwa kortini leo .