Kenya hii leo imesajili visa 141 vipya vya maambukizi ya corona huku maambukizi ya maradhi hayo yakifikia 100,193
Hii ni baada ya sampuli 3,571 kupimwa chini ya saa 24.
Kati ya maambukizi hayo mapya 121 ni wakenya huku 20 wakiwa raia wa kigeni.
81 ni wanaume huku 60 wakiwa ni wanawake,mgonjwa wa umri wa chini ana mwaka mmoja huku mwenye umri wa chini akiwa na miaka 87.
Vile vile watu 207 wamepona virusi hivyo na kufikisha idadi jumla ya 83,625 ya watu waliopona corona.
Watu 192 wamepona wakiwa wanapokea matibabu wakiwa nyumbani huku 15 wakiruhusiwa kuenda nyumbani kutoka hospitali tofauti nchini.
Wagonjwa 500 wamelazwa hospitalini tofauti humu nchini huku 1,340 wakiwa wamejitenga nyumbani.
Huku hayo yakijiri watu 6 amepoteza maisha yake kutokana na corona na kufikisha idadi jumla ya 1,750 watu waliada kutokana na corona
Pia wagonjwa 25 wamo katika wadi wa wagonjwa mahututi (ICU).