- Watahiniwa 1,191,411 wamesajili kufanya mtihani wa KCPE katika vituo 28,451
- Watahiniwa 752,933 wamesajiliwa kufanya KCSE katika vituo 10,437 ikilinganishwa na vituo 10,287 mwaka wa 2019
Kutakuwa na idadi kubwa ya maafisa watakaotumwa katika vituo vya mitihani ya kitaifa ili kuhakikisha kwamba inafanywa kwa ufanisi hasa kwa ajili ya janga la sasa la Corona
Baraza la kitaifa la mtihani KNEC limesema Zaidi ya maafisa 286,901 wa nyanjani watatumiwa kusimamia mitihani hiyo ikilinganishwa na idadi ya maafisa 173,000 waliotumiwa mwaka wa 2019 .
Maelezo hayo yamo katika ripoti ya matayarisho ya kufanywa kwa mitihani ya kitaifa . mitihani ya mwaka huu ya KCPE na KCSE itafanywa mwezi machi na Aprili .kwa kawaida mitihani hiyo hufanywa kati ya Oktoba na Novemba .
Watahiniwa 1,191,411 wamesajili kufanya mtihani wa KCPE katika vituo 28,451
Watahiniwa 752,933 wamesajiliwa kufanya KCSE katika vituo 10,437 ikilinganishwa na vituo 10,287 mwaka wa 2019
Kufuatia kipindi kirefu ambapo shule zilifungwa KNEC intarayarisha takwimu za shule ambazo zilifungwa na watahiniwa kuathiriwa . Miongoni mwa changamoto ambazo huenda zikatokea wakati wa mitihani hiyo ni msimu wa mvua . Baraza la mtihani pia linahofia hali mbaya ya usalama na mafuriko katika maeneo kadhaa huenda zikasababisha usumbufu wakati wa mtihani .
Katika mitihani ya mwaka huu knec imetumia kontena 479 katika makao makuu ya kaunti ndogo ili kuhifadhi karatasi za mtihani .