Viboko Shuleni

Knut yaapa kupinga kurejeshwa kwa adhabu ya viboko shuleni

Ameitaka serikali kuziondoa shule za mabweni ili kila mzazi atekeleze jukumu la kumuadhibu mtoto wake .

Muhtasari

 

  •  Waziri wa elimu George Magoha wiki jana alipendekeza kurejeshwa kwa dhabu ya viboko shuleni ili kukabiliana na visa vya ukosefu wa nidhamu miongoni mwa wanafunzi .
  •  Waziri huyo pia alilalamikia ongezeko la visa vya wanafunzi kuzichoma shule zao na  kuwashambulia walimu .
Katibu mkuu wa KNUT Wilson Sossion

 Muungano wa walimu nchini KNUT umeapa kupinga kurejeshwa kwa adhabu ya kuchapwa viboko shuleni  ukisema hatua hiyo italeta malumbano kato ya walimu na wanafunzi .

 Katibu mkuu wa KUT Wilson Sossion amesema  kurejeshwa kwa adhabu hiyo kutahatarisha maisha ya walimu hasa kutoka kwa wanafunzi ambao sasa ndio wanaingia umri wa kubaleghe 

 Ameitaka  serikali kuziondoa shule za mabweni ili kila mzazi atekeleze jukumu la kumuadhibu mtoto wake .

Sossion  wakati huo huo pia ameishtumu serikali kwa kuifanya dhaofu miungano ya wafanyikazi  ili kuwatumia vibaya wafanyikazi .Amemtaka rais Uhuru Kenyatta  kuingilia kati ili kumaliza malumbano kati ya KNUT na TSC .

 Waziri wa elimu George Magoha wiki jana alipendekeza kurejeshwa kwa dhabu ya viboko shuleni ili kukabiliana na visa vya ukosefu wa nidhamu miongoni mwa wanafunzi .

 Waziri huyo pia alilalamikia ongezeko la visa vya wanafunzi kuzichoma shule zao na  kuwashambulia walimu .

‘Adahabu ya viboko ikitumiwa vizuri inaweza kupunguza kabisa visa vya utovu wa nidhamu miongoni  mwa wanafunzi ‘ alisema Magoha .

Aliwashauri wazazi  kupambana na wanao wakiwa nyumbani ili kupunguza utundu wao wakiwa shuleni .