Simeon Nyachae

Familia ,Viongozi wamkumbuka Nyachae kama kiongozi aliyekuwa na maono

Nyachae aliwahi kuhudumu kama waziri Fedha ,Kawi na baadaye Barabara na ujenzi wa umma .

Muhtasari
  •  Mwanasiasa huyo aliyehudumu kama  mkuu wa mkoa  amekuwa hospitali kwa muda wa  Zaidi ya mwezi mmoja  .
  •  Rais alisema mbunge huyo wa zamani wan Nyaribari Chache alikuwa mtu mcheshi ,alipatikana kwa urahisi na mzee wa kutegemewa

 

Simeon-Nyachae
Marehemu Simeon Nyachae Simeon-Nyachae

  Familia na marafiki wa  waziri wa zamani  Simeon Nyache wamemtaja kama kiongozi ambaye alikuwa na maono makubwa na  aliyekuwa akifuata kila kanuni za nidhamu . Nyanchae ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 88 .

 Wake zake wawili Martha na Grace walijawa na huzuni wakati walipofika katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Lee . Mwanawe ,mwenyekiti wa  iliyokuwa tume ya  kiutekeleza katiba Charles Nyachae  na waziri wa usalama wa ndani Fred Matiang’I  waliongoza familia katika kutangaza kifo cha  Simeon Nyachae .

" Sote tumempoteza  baba na kielelezo’ Matiang’I alisema baada ya Charles kutoa Habari  za  kifo cha babake .

 

 Mwanasiasa huyo aliyehudumu kama  mkuu wa mkoa  amekuwa hospitali kwa muda wa  Zaidi ya mwezi mmoja  . Familia yake imesema aliaga dunia kutokana na ugonjwa  ambao amepambana  na ‘kwa ujasiri’

 Rais Uhuru Kenyatta amemtaja Nyachae kama  kielelezo cha maendeleo nchini  kupitia miaka yake mingi katika utumishi wa umma . Kupitia taarifa Uhuru  alijutia kifo cha Nyachae akisema kwamba alikuwa kiongozi wa taifa mwenye busara  ambaye utumishi kwa nchi uliaidia kuifanya Kenya kuwa kitovu cha ustawi katika bara la  Afrika .

 Rais alisema mbunge huyo wa zamani wan Nyaribari Chache alikuwa mtu mcheshi ,alipatikana kwa urahisi na mzee wa kutegemewa

 Katibu wa usimamizi wa wizara ya Uchukuzi na miundo msingi alikitaja kifo cha Nyache kama hatua ambayo imeacha jamii ya Gusii  katika hali mbaya .

  Rais wa zamani Mwai Kibaki amemtaja Nyache kama mmoja wa watumishi wenye bidii wa umma Kenya . Nyachae aliwahi kuhudumu kama waziri Fedha ,Kawi na baadaye  Barabara na ujenzi wa umma .