Polisi huko Laikipia wanachunguza tukio la mauaji ya mwanamke mwenye umri wamiaka 43 katika kijiji cha Ngobit . Mwili wake ulipatikana katika chumba chake cha kulala na inashukiwa aliuawa na watu waliomkata shingoni na kutoroka .
Kisu kilichokuwa na damu kimepatikana kando ya mwili wake .mwanamke huyo alikuwa akiishi karibu na baa moja ambako alikuwa akifanya kazi .Makachero wanaucnguza tukio hilo wanalenga kubaini kilichosababisha mauaji yake .mwili wake umepelekwa katika hifadhi ya maiti .