MCK yalaani vikali mashambulio dhidi ya wanahabari,waliokuwa wakiripoti maandamano ya Azimio

Omwoyo alisema maafisa wa polisi kuwashambulia wanahabari kunadhoofisha uhuru wa vyombo vya habari,

Muhtasari
  • Mkurugenzi Mtendaji wa MCK David Omwoyo alisema waandamanaji wanaoshambulia vyombo vya habari wanadhalilisha
Mkurugenzi mkuu wa MCK, David Omwoyo
Image: MCK (Facebook)

Baraza la Vyombo vya Habari nchini (MCK) limelaani ghasia zilizofanywa dhidi ya wanahabari waliokuwa wakiripoti maandamano siku ya Jumatatu.

Waandishi wa habari kutoka vyombo vya habari vya humu nchini na kimataifa walishambuliwa na genge la watu wenye visu huko Kibra, huku wengine kadhaa wakijeruhiwa baada ya gengekurushia magari yao mawe.

Vifaa vya thamani pia vilipotea katika matukio hayo. Kupitia taarifa, Mkurugenzi Mtendaji wa MCK David Omwoyo alisema waandamanaji wanaoshambulia vyombo vya habari wanadhalilisha ari ya kuchukua hatua kwa watu wengi kwani inasaliti misingi ya demokrasia ambayo imeanzishwa.

"Kupanga hatua ya watu wengi ambayo huanza kwa kushambulia vyombo vya habari ni kushindwa na ni hatari kwa maadili ya kidemokrasia," alisema.

Omwoyo alisema maafisa wa polisi kuwashambulia wanahabari kunadhoofisha uhuru wa vyombo vya habari, kuweka mipaka kwa umma kupata habari, kukiuka haki za binadamu na kunaweza kusababisha madhara ya kimwili au kisaikolojia.

“Ni muhimu kwamba waandishi wa habari wawe na uwezo wa kufanya kazi yao bila kuogopa vurugu au unyanyasaji, na kwamba vyombo vya kutekeleza sheria viwajibike kwa vitendo vyovyote vinavyokiuka haki zao. au kuzuia uwezo wao wa kuripoti matukio,” alisema bosi huyo wa shirika la uangalizi wa vyombo vya habari.

Baraza lilisema litafanya kazi kwa karibu na vyombo vya kutekeleza sheria ili kuhakikisha waliohusika na mashambulizi hayo wanawajibishwa kwa vitendo hivyo, na kuhakikisha matukio kama hayo yanazuiwa katika siku zijazo.

"Tunawapongeza na kusimama katika mshikamano na wanahabari wote wanaojiweka hatarini kuripoti matukio na kuwafahamisha umma, na tunasisitiza dhamira yetu ya kutetea vikali uhuru wa vyombo vya habari," iliongeza taarifa hiyo.