Wanafamilia 4 wafariki baada ya lori kupoteza mwelekeo Bungoma

Walikuwa wamehudhuria mazishi ya wapendwa wao katika Kaunti ya Bungoma.

Muhtasari

•Waliofariki ni wanawake wawili na wanaume wawili waliokuwa wakisafiri kwa pikipiki wakielekea njia ya Kanduyi.

•Gavana Barasa alisema marehemu wanatoka eneo la jamii ya Machemo, wadi ya Chemuche eneo bunge la Malava kaunti ya Kakamega.

Ajali
Ajali
Image: HISANI

Wakaazi wa soko la Mayanja Kibuke, kaunti ya Bungoma waliachwa na mshtuko mkubwa Jumapili baada ya trela kuacha barabara na kuwaua wanafamilia wanne.

Akizungumza Jumapili, Patrick Masika alisema kuwa marehemu walikuwa wakisafiri kurejea nyumbani Malava kaunti ya Kakamega.

Walikuwa wamehudhuria mazishi ya wapendwa wao katika Kaunti ya Bungoma.

Masika alisema waliofariki ni wanawake wawili na wanaume wawili waliokuwa wakisafiri kwa pikipiki wakielekea njia ya Kanduyi.

"Tumeshuhudia ajali mbaya sana hapa, ni wito wetu kwa KeNHA kuweka matuta barabarani ili kuzuia ajali za mara kwa mara," alisema.

Masika alisema kuwa watu wengi wamepoteza maisha katika barabara hiyo hiyo lakini mamlaka husika hazijachukua hatua ya kuweka matuta (bampu) kwenye barabara hiyo yenye shughuli nyingi.

Alisema wakazi wa soko la Mayanja hawakuweza kuwatambua marehemu.

Gavana wa Kakamega Fernandez Barasa, katika risala ya rambirambi iliyofikia Radio Jambo, alisema kuwa marehemu wanatoka eneo la jamii ya Machemo, wadi ya Chemuche eneo bunge la Malava kaunti ya Kakamega.

“Nimesikia kwa huzuni kubwa kifo cha wakazi wanne wa Kaunti ya Kakamega walioangamia kwenye ajali ya barabarani katika kituo cha biashara cha Mayanja kando ya barabara ya Malaba-Eldoret walipokuwa wakirejea nyumbani baada ya kumnunua mpendwa wao katika Kaunti ya Bungoma,” akasema. .

Barasa aliwaonya watumiaji wa barabara kuwa waangalifu ili kuepusha ajali hizo siku zijazo.