Mwanabodaboda auawa kwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mke wa kasisi

Kasisi huyo, mkewe na watoto wanaripotiwa kutoroka nyumbani.

Muhtasari
  • Kulingana na Chifu Andrew Ombisa wa eneo hilo, marehemu anasemekana kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mke wa kasisi huyo kwa muda mrefu.
Crime Scene
Image: HISANI

Mwendesha bodaboda mwenye umri wa miaka 38 ameuawa kwa sababu ya kuwa kwenye mapenzi na mke wa kasisi katika kijiji cha Kumbatha, eneo dogo la Seka eneo la Gwasii Mashariki katika eneo bunge la Suba Kusini.

Marehemu, aliyetambulika kama Wilson Onjiro Otieno, anaripotiwa kwenda kwa nyumba ya kasisi huyo Jumapili usiku kukutana na mkewe (kasisi) bila kutambua kuwa kasisi huyo alikuwa ndani ya nyumba hiyo.

Kulingana na Chifu Andrew Ombisa wa eneo hilo, marehemu anasemekana kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mke wa kasisi huyo kwa muda mrefu.

Kulingana na Citizen Digital Inasemekana alikuwa akitumia fursa ya kutokuwepo kwa kasisi huyo alipokuwa nje kwa shughuli za kiroho katika Kitongoji cha Sindo ili kulala na mkewe katika kitanda chao cha ndoa.

Chifu anaripoti kuwa zogo kati ya mtu wa Mungu na marehemu lilianza pale mwanamume huyo aliyeonekana kuwa mlevi aliingia ndani ya nyumba hiyo bila ya kuona uwepo wa padri huyo.

Baada ya mabishano ya muda mrefu, marehemu alikwenda nyumbani kwake na kurejea akiwa na silaha ghafi ili kumshambulia kiongozi huyo wa dini. Kasisi huyo alitoa simu yenye huzuni iliyowatahadharisha watu ambao walimwua mvamizi huyo.

Ombisa anasema mwendesha bodaboda huyo aliuawa katika boma hilo kabla ya mwili wake kukokotwa hadi shule ya msingi ya Kumathi ambako ulipatikana Jumatatu asubuhi.

Kasisi huyo, mkewe na watoto wanaripotiwa kutoroka nyumbani.