Mshtuko huku mfanyibiashara akijipiga risasi ndani ya gari lake Lang'ata

Sababu ya tukio hilo bado haijajulikana, polisi walisema.

Muhtasari

•Abraham Meli alikuwa amejifungia ndani ya gari lake la magurudumu manne- Prado- na kupata jeraha mbaya la risasi kichwani.

•Alikimbizwa katika Hospitali ya St Mary ambapo alitangazwa kuwa amefariki baada ya polisi kuwasili.

Marehemu Abraham Meli
Image: HISANI

Polisi wanachunguza kisa ambapo mfanyibiashara mmoja alidaiwa kujipiga risasi na kufa akiwa ndani ya gari lake, katika kile kinachoonekana kuwa kisa cha kujitoa uhai katika mtaa wa Sunvalley, Lang'ata, Nairobi.

Abraham Meli alikuwa amejifungia ndani ya gari lake la magurudumu manne- Prado- na kupata jeraha mbaya la risasi kichwani.

Sababu ya tukio hilo bado haijajulikana, polisi walisema.

Meli ni mwanajeshi wa zamani na alikuwa na leseni ya mmiliki wa bunduki, familia yake na polisi walisema.

Alikimbizwa katika Hospitali ya St Mary ambapo alitangazwa kuwa amefariki baada ya polisi kuwasili.

Bastola yake ilipatikana ndani ya gari ambapo alikuwa amejipiga risasi na ikapelekwa chini ya ulinzi, polisi walisema.

Polisi walisema alikuwa ametuma ujumbe mfupi wa simu kwa jamaa uliosomeka "Sunvalley". Hapa ni mahali pale alipokaa.

Polisi walisema wanachunguza tukio hilo ili kubaini chanzo. Marafiki na familia yake wanatafuta kuelewa motisha nyuma ya matendo yake.

Mwili wake ulisafirishwa hadi katika chumba cha kuhifadhia maiti ukisubiri kufanyiwa uchunguzi. Polisi walisema sasa wanachukulia tukio hilo kama la kujitoa mhanga.

Hiki kinaashiria kisa cha hivi majuzi zaidi cha kujiua.