Mwanamume anayedaiwa kumlalamikia mkewe kwenye Twitter na kumuua apatikana amefariki

Mwili wa Evans Kosgei ulipatikana ukining'inia kutoka kwa mti ukiwa na kamba shingoni.

Muhtasari

•Evans Kosgei anashukiwa kufariki kwa kujitoa uhai Jumapili usiku au Jumatatu asubuhi, polisi walisema.

•Kosgei anaripotiwa kumuua Jackline katika sakata ya mzozo wa mapenzi.

Mwanamume anayedaiwa kumuua mkewe Mathira na kuandika kwenye Twitter apatikana amekufa

Evans Kosgei ambaye alimuua mkewe kabla ya kudaiwa kujitoa uhai.
Image: HISANI

Mwanamume aliyedaiwa kumuua mke wake katika eneo la Mathira kaunti ya Nyeri alipatikana akiwa amefariki baada ya kujitoa uhai katika eneo la Thika, kaunti ya Kiambu.

Mwili wa Evans Kosgei ulipatikana ukining'inia kutoka kwa mti ukiwa na kamba shingoni mnamo siku ya Jumatatu, Machi 11, polisi walisema.

Anashukiwa kufariki kwa kujitoa uhai Jumapili usiku au Jumatatu asubuhi, polisi walisema.

Mwili wake ulipatikana kwenye mti muda mrefu baada ya kukwepa nyavu za polisi katika eneo la Jomoko kwenye barabara ya Thika-Mangu.

Alipatikana na kitambulisho cha mwenziwe aliyekufa Jackline Jerop Kimaiyo na barua iliyoonyesha kuwa alihusika na mauaji ya wenzi wake.

Ujumbe wa kujitoa uhai ulichukuliwa kwa ajili ya uchunguzi. Alikuwa ametoweka tangu Machi 6 wakati mwili wa mkewe na mama wa mtoto mmoja ulipopatikana katika eneo la Mathira baada ya mauaji anayohusishwa nayo.

Mwili wake ulichukuliwa na kuhifadhiwa katika mochari General Kago mjini Thika.

Kosgei anaripotiwa kumuua Jackline katika sakata ya mzozo wa mapenzi.

Alikuwa mwalimu katika eneo la Mathira Mashariki ambapo mwili wake ulipatikana wakati mumewe akiwa mlinzi wa usiku katika eneo la Thika.

Aliishi Waitethie, Thika takriban kilomita 50 kutoka ambapo mke alifanya kazi.

Kabla na baada ya Jackline kuuawa kikatili, Kosgei alikuwa ameingia kwenye mitandao ya kijamii na kumshutumu kwa kum’cheat.

Kundi la polisi kutoka Nyeri lilikuwa likifuatilia mienendo yake na kufichua kuwa alikimbilia Mombasa kwa kile wanachoamini kuwa ni matambiko.

Alivuka kivuko hadi Likoni ambako alikaa kwa siku mbili kabla ya kurejea Jumamosi usiku.

Kulingana na polisi, Kosgei kila mara alizima simu yake ya rununu kila alipokuwa kwenye harakati na kuzima SIM kadi yake muda wote ili asigunduliwe.

Maafisa wa upelelezi wanaofahamu kisa hicho walisema wamekuwa wakishirikiana na wenzao katika makao makuu kumsaka mshukiwa huyo bila mafanikio.

Siku ya Jumapili, aliwasha simu yake ya rununu kwa dakika chache akiwa Thika kabla ya kuzima tena.

Pia alikuwa akitafutwa katika sehemu yake ya kazi na hivyo alikuwa amefanya mipango yote muhimu kwa ajili ya mienendo yake.

Timu iliyokuwa ikimfuata ilisema ilipiga kambi katika eneo la Thika kati ya makazi yake na mahali pa kazi bila mafanikio.

"Tulijua suala hilo lilikuwa kwenye mitandao ya kijamii na kila mtu alikuwa akifuata mkondo wake lakini hatukuweza kufanya lolote kusaidia," afisa anayefahamu suala hilo alisema.

Kulingana na mitandao ya kijamii, Kosgei alimshutumu Jackline kwa kupanga kumtema licha ya kuuza kila kitu ili kumlipia karo ya shule katika Chuo Kikuu cha Murang'a.

Katika mfululizo wa Tweets, Kosgei aliahidi "kujiunga" na mke wa marehemu kwa sababu, kwake, maisha yalikuwa yamepoteza maana.

Kosgei alitumia akaunti yake ya X, kutoa taarifa za kutisha zilizoelekezwa kwa mwenzi wake, hata kutambulisha mamlaka za kutekeleza sheria na vyombo vya habari.