•Sakaja aliapishwa kama gavana wa nne wa Nairobi mwendo wa saa tano asubuhi ya Alhamisi katika ukumbi wa KICC.
•Aliwasili katika ukumbi huo mwendo wa saa nne unusu asubuhi akiwa ameandamana na familia yake.
Aliyekuwa seneta wa Nairobi Johnson Sakaja ameapishwa kama gavana wa nne wa kaunti hiyo.
Sakaja aliapishwa mwendo wa saa tano asubuhi ya Alhamisi katika ukumbi wa KICC.
Hakimu Roselyn Aburili ndiye aliyesimamia hafla hiyo.
Mamia ya wageni waalikwa wakiwemo wanasiasa mashuhuri walishuhudia kuapishwa kwa Sakaja moja kwa moja. Rais mteule William Ruto ni miongoni mwa wageni waliokuwa wamehudhuria.
Sakaja aliwasili katika ukumbi huo mwendo wa saa nne unusu asubuhi akiwa ameandamana na familia yake. Alikuwa amevalia suti ya bluu bahari na tai nyekundu huku wanawe wakiwa na suti ya kijivu na tai nyeusi.
Mke wake Beatrice Sakaja, wanawe wawili waliongozana naye kwenye hafla hiyo. Binti aliyekuwa pamoja nao sio wake.