Mlinzi wa klabu ya Watford Adrian Marriapa akiri kuwa na Corona

EYh44chWAAEuihY
EYh44chWAAEuihY

Mlinzi wa Klabu ya Watford Adrian Marriapa wa miaka 33 amekiri kuwa baada ya kufanyiwa vipimo na madaktari wa klabu hiyo alipatikana na virusi vya corona.

Jumanne taarifa zilidai kuwa wachezaji sita wa ligi kuu ya Uingereza pamoja japo majina ya wacheazji hao na timu zao hayakufichuliwa kamwe.

Marripa amesema ni miongoni mwa wachezaji watatu wa klabu hiyo ambao wameathirika.

Kiungo wa Chelsea Ngolo Kante alikosa kuhudhuria mazoezi kwa siku ya kwanza kutokana na hofu kuwa ataambukizwa virusi hivyo, swala ambalo mkufunzi Lampard alimuunga mkono.

Hatua ya Kante kusalia nyumbani wakati wachezaji wenza wanapoendelea na mazoezi imeambatana na uamuzi wa mchezaji Troy Deeney ambaye alitupilia mbali uwezekano wake wa kurejea kucheza wakati Uingereza inakabiliana na virusi hivyo.

Marriapa amesema amesikitishwa na matokeo hayo akisema amekuwa akifanya mazoezi yake nyumbani na hakuna siku hata moja aliyotoka nje ya boma lake.

"Apart from some exercise and the odd walk with the kids, I've mainly just been homeschooling and keeping fit."My lifestyle is very quiet, certainly no parties or going out or anything, so I really don't know how I got it."amesema Marripa

Aliongezea kuwa hakuonyesha dalili zozote za virusi hivyo na swala hilo limemshangaza