Ufaransa V Morocco: Je nani kutinga fainali dhidi ya Argentina?

Mara nyingi sana kwenye michuano hii, tunapuuza timu kutoka nje ya Ulaya na Amerika Kusini.

Muhtasari

• "Mashabiki wa Argentina waliiburuza timu yao katika mechi - ilikuwa kama mchezo wa nyumbani kwao dhidi ya Uholanzi katika nane bora, na ikawa vivyo hivyo dhidi ya Croatia.

Kylian Mbappe na Hakim Ziyech
Kylian Mbappe na Hakim Ziyech
Image: BBC SPORT

Mashabiki wa  Morocco ndio wamekuwa na kelele zaidi kwenye Kombe hili la Dunia lakini wanaweza kusaidia timu yao kushinda nusu fainali dhidi ya Ufaransa?

"Ningependa kuona Morocco ikifanikiwa, kwa sababu ya usaidizi wa ajabu wa timu hiyo," mtaalam wa soka wa BBC Sport Chris Sutton alisema.

"Mashabiki wa Argentina waliiburuza timu yao katika mechi - ilikuwa kama mchezo wa nyumbani kwao dhidi ya Uholanzi katika nane bora, na ikawa vivyo hivyo dhidi ya Croatia.

"Nikiwa na Morocco, pia nadhani itakuwa hadithi nzuri kwa timu ya Afrika kufanya hivyo. Mara nyingi sana kwenye michuano hii, tunapuuza timu kutoka nje ya Ulaya na Amerika Kusini, lakini Morocco imewafanya watu kuwa na fikra tofauti .

"Watakuwa chaguo langu la kimapenzi kutinga fainali, lakini sina uhakika sana kuhusu nafasi zao dhidi ya Ufaransa."

Sutton anatabiri matokeo ya kila mechi nchini Qatar.

Alichagua  mshindi katika mechi mbili kati ya nne za robo fainali - akipata alama kamili katika ushindi wa Morocco dhidi ya Ureno na ushindi wa Ufaransa dhidi ya Uingereza - na mechi tano kati ya nane za 16 bora.

Hiyo ilitosha kudumisha kiwango chake cha mafanikio cha 55% katika dimba hilo, baada ya kuchagua matokeo sahihi katika michezo 26 kati ya 48 ya kundi.

Kabla ya Kombe la Dunia kuanza, Sutton alichagua timu 12 kati ya 16 zilizofuzu kwa hatua ya kwanza ya mtoano, ikiwa ni pamoja na Ufaransa, chaguo lake la kushinda michuano hiyo, na Uingereza, ambayo alisema kwa usahihi itatinga hadi nane bora.

Kylian Mbappe na Hakim Ziyech
Kylian Mbappe na Hakim Ziyech
Image: BBC SPORT
Kylian Mbappe na Hakim Ziyech
Kylian Mbappe na Hakim Ziyech
Image: BBC SPORT