Beki wa Morocco na PSG Achraf Hakimi matatani kwa tuhuma za ubakaji

Inaarifiwa beki huyo wa miaka 24 aliingia nyumbani kwa mwanadada wa miaka 23 na kumbaka.

Muhtasari

• Tayari uchunguzi umeanzishwa lakini Sio Hakimi wala PSG wamejibu hadharani shutuma hizo.

Beki Achraf Hakimi matatani kwa tuhuma za ubakaji.
Beki Achraf Hakimi matatani kwa tuhuma za ubakaji.
Image: BBC SPORT.

Waendesha mashtaka wa Ufaransa wamefungua uchunguzi wa awali kuhusu tuhuma ya ubakaji iliyofanywa na mlinzi wa Morocco Achraf Hakimi, chanzo kilicho karibu na uchunguzi kimethibitisha.

Mwanamke mwenye umri wa miaka 24 amemshutumu beki wa pembeni wa Paris St-Germain kwa kumbaka nyumbani kwake katika mji mkuu wa Ufaransa tarehe 25 Februari.

Chanzo hicho kilisema mwanamke huyo aliripoti tukio hilo katika kituo cha polisi siku ya Jumapili lakini hakufungua mashtaka. Ofisi ya mwendesha mashtaka wa umma inayoshughulikia kesi hiyo huko Nanterre, katika viunga vya magharibi mwa Paris, ilikataa kutoa maoni lakini ilithibitisha kuwa uchunguzi umeanza, BBC Sport waliripoti.

Uchezaji wake ulimwezesha kutunukiwa katika hafla ya Tuzo Bora za Kandanda za Fifa zilizofanyika jijini Paris Jumatatu jioni, ambapo aliteuliwa katika timu ya mwaka ya dunia ya mwaka ya FIFPro ya wanaume.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alisimama jukwaani kuchukua tuzo hiyo pamoja na washindi wengine wakiwemo wachezaji wenzake wa PSG Kylian Mbappe na Lionel Messi.

Sio Hakimi wala PSG wamejibu hadharani shutuma hizo.

Hakimi alizaliwa Uhispania, alikuwa mchezaji muhimu wakati Morocco iliweka historia kwa kufika nusu fainali ya Kombe la Dunia nchini Qatar, timu ya kwanza ya Kiafrika kufanya hivyo.

Walianzisha uchunguzi kutokana na uzito wa tuhuma hizo na sifa mbaya ya Hakimi.

Kulingana na Le Parisien, beki huyo mwenye umri wa miaka 24 alianza kuzungumza na mwanamke huyo mnamo Januari 16 kwenye Instagram.