Ilinichukua miezi sita kutulia Man Utd - Onana

United walilipa £47.2m kumsajili Onana kutoka Inter Milan mwezi Julai kuchukuwa nafasi ya kipa Mhispania David de Gea.

Muhtasari
  • Hofu ya baadhi ya mashabiki wa United kuhusu mechi ya fainali ya Kombe la FA kwa mara ya pili mfululizo dhidi ya Manchester City inatokana na idadi kubwa ya nafasi inayopotezwa na timu yao.
Kipa wa Manchester United Andre Onana
Image: MAKTABA

Kipa wa Manchester United Andre Onana anasema ilimchukua miezi sita "kutulia" Old Trafford.

United walilipa £47.2m kumsajili Onana kutoka Inter Milan mwezi Julai kuchukuwa nafasi ya kipa Mhispania David de Gea.

Hata hivyo, licha ya matarajio makubwa juu ya ujio wake, mchezaji huyo wa kimataifa wa Cameroon alifungwa kwa umbali wa yadi 50 katika mechi yake ya kwanza Old Trafford dhidi ya Lens na kisha akafanya makosa kadhaa ambayo yalichangia klabu hiyo kutofanya vizuri katika Ligi Kuu na kuondolewa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa.

Uchezaji wa Onana haukuimarika sana hadi aliporejea kutoka Kombe la Mataifa ya Afrika mwezi Februari na ingawa amefanya makosa ya ajabu, sasa anachukuliwa kuwa mmoja wa wachezaji wa kutegemewa wa kikosi cha meneja Erik ten Hag watakapoelekea Jumamosi

Fainali ya Kombe la FA dhidi ya wapinzani Manchester City (15:00 BST). “Nilifika nikiwa kipa bora zaidi duniani na ‘boom’ ilishuka.

Ilikuwa kama ‘nini kilitokea?’,” alisema kijana huyo mwenye umri wa miaka 28. “Lakini hivyo ndivyo soka linavyokuwa gumu wakati mwingine.

Inategemea kama unataka kukaa chini na kulia au kusimama na kupigana.

Najua nilichokifanya kufika hapa. Najua mimi ni nani. Niliamua kusimama na kupigana.”

Onana anatoa mfano wa mchezaji mwenza Marcus Rashford kwa nini wachezaji wanahitaji kuepuka kuwahukumu vikali wenzao.

Rashford alifunga mabao 30 msimu uliopita. Msimu huu, ameongoza timu mara nane na hakufanikiwa hata kuteuliwa kwa kikosi cha muda cha wachezaji 33 cha Kocha wa Uingereza Gareth Southgate cha Ubingwa wa Ulaya, achilia mbali mchujo wa mwisho.

"Tunazungumza juu ya mchezaji mmoja," Onana alisema. "Kwa hiyo sasa yeye ni mchezaji mbaya? Hapana. Unaweza kuwa na msimu mbaya au mwanzo mbaya lakini la muhimu zaidi ni jinsi unavyomaliza.

"Rashy, kwangu, ni mmoja wa wachezaji bora zaidi ulimwenguni. Lakini anakabiliwa na ugumu. Sio mimi na yeye pekee bali klabu nzima.

“Lakini atakuwa sawa. Najua nyota wangu atatufungia mabao muhimu. Natumai atafunga mabao mawili dhidi ya City na tutashinda Kombe la FA.”

Hofu ya baadhi ya mashabiki wa United kuhusu mechi ya fainali ya Kombe la FA kwa mara ya pili mfululizo dhidi ya Manchester City inatokana na idadi kubwa ya nafasi inayopotezwa na timu yao.

Kulikuwa na mfululizo wa mechi saba kati ya Machi na Aprili ambapo wapinzani waliotea lango la Onana karibu mara 20 katika kila mechi.

Walipocheza na City mara ya mwisho mwezi Machi, walipiga mashuti matatu kwa wapinzani wao 27 kati ya hizo zikigonga mwamba na kuwafanya kushindwa 3-1.

Onana anahisi matokeo hayo yalimfanya Ten Hag kulazimika kufanya kwenye safu yake ya ulinzi.

Ushirikiano kati ya Casemiro na Lisandro Martinez ulioanza huko Brighton mnamo 19 Mei ulikuwa wa 15 wa safu ya ulinzi ya kati United kutumwa msimu huu. Hakuna ushirikiano ambao umeanza zaidi ya michezo minne mfululizo.

"Sijali kuzuia mabao 20 au 30," Onana alisema. "Nimefurahishwa sana na kile wachezaji wenzangu wanafanya kwa sababu wengi wao hujitolea kwa ajili ya timu.

"Ingekuwa vyema kama kila mmoja angeshiriki lakini tuna la kufanya kweli? ama tujifiche? Sisi ni klabu kubwa. Tunapaswa kuwa wajasiri wa kukabiliana na matatizo. Nina imani. Najua mambo yatakuwa mazuri. Kama si leo, kesho.”