Ian Maatsen na Hakim Ziyech waondoka Chelsea kwa uhamisho wa kudumu

Uamuzi wa Chelsea wa kuwauza Maatsen na Ziyech unalingana na mtazamo wao wa kimkakati wa kupanga upya na kusawazisha kikosi.

Muhtasari

• Galatasaray haikuchukua ada ya mkopo kwa Ziyech msimu uliopita lakini ililipa mshahara wake, ambao ni €3.5m. Kwa msimu ujao, mshahara wa Ziyech umebadilishwa hadi €2.8m.

• Mkataba wa mwaka mmoja unajumuisha chaguo la msimu wa ziada, kulingana na hali ambayo haijabainishwa

Ian Maatsen na Hakim Ziyech
Ian Maatsen na Hakim Ziyech
Image: CHELSEA

Chelsea wamekamilisha kumuuza Ian Maatsen kwa Aston Villa kwa kitita cha pauni milioni 38 ($48m) huku Hakim Ziyech akijiunga na Galatasaray.

Mkataba wa awali wa Maatsen huko Chelsea ulitarajiwa kumalizika Juni 2025. Hata hivyo, uliongezwa kwa miezi 12 zaidi mnamo Januari kabla ya uhamisho wake wa mkopo kwenda Dortmund.

Huko Ujerumani, alibadilika haraka na kujiweka kama sehemu muhimu ya timu. Katika kipindi chake akiwa Dortmund, Maatsen alitoa mchango mkubwa, akianza mechi zao zote saba za Ulaya, ikiwa ni pamoja na fainali ya Ligi ya Mabingwa, na kushirikisha mechi 15 kati ya 18 za Bundesliga.

Kando na uhamisho wa Maatsen, Chelsea ilithibitisha kuondoka kabisa kwa Hakim Ziyech kwenda Galatasaray.

Winga huyo wa Morocco alitumia msimu uliopita kwa mkopo na wababe hao wa Uturuki, ambapo kipengele kilijumuishwa kufanya uhamisho huo kuwa wa kudumu.

Kifungu hiki sasa kimeamilishwa bila gharama na Ziyech ataendelea na taaluma yake nchini Uturuki.

Licha ya majeraha ya mguu na kifundo cha mguu kutatiza kampeni yake, alifanikiwa kucheza mechi 23 katika mashindano yote, akifunga mabao nane na kutoa asisti nne.

Galatasaray haikuchukua ada ya mkopo kwa Ziyech msimu uliopita lakini ililipa mshahara wake, ambao ni €3.5m. Kwa msimu ujao, mshahara wa Ziyech umebadilishwa hadi €2.8m.

Mkataba wa mwaka mmoja unajumuisha chaguo la msimu wa ziada, kulingana na hali ambayo haijabainishwa.

Meneja wa Villa, Unai Emery, amekuwa akimpenda Maatsen kwa muda mrefu. Huku Villa wakijiandaa kwa kampeni yao ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa, Emery alimtambua beki huyo mchanga kama nyongeza muhimu kwenye kikosi chake.

Uamuzi wa Chelsea wa kuwauza Maatsen na Ziyech unalingana na mtazamo wao wa kimkakati wa kupanga upya na kusawazisha kikosi.

Klabu hiyo inalenga kuboresha orodha yao huku ikihakikisha kuwa na busara ya kifedha na uuzaji wa Maatsen utawafanya wapate faida ambayo itakuwa muhimu katika juhudi zao za kufuata kanuni za faida na uendelevu za Ligi ya Premia (PSR).