Baada ya kumpiga kalamu Unai Emery, Arsenal wataandikisha ushindi leo?

Klabu ya Arsenal hii leo watakuwa wanachuana na Brighton katika ligi ya Uingereza.

Arsenal walisitisha ukufunzi wa Unai Emery wiki jana baada ya matokeo duni katika msimu huu na kwa sasa wanashikilia nafasi ya 10 wakiwa na pointi 19.

 Katika mchuano uliopita dhidi ya Norwich, Arsenal waliambulia sare ya mabao mawili, na hii leo watakuwa wanategemea huduma ya washambulizi wao Pierre-Emerick Aubameyang, Alexandre Lacazette, na Nicholas Pepe kushinda mechi hiyo.

Brighton kwa upande wao wanashikilia nafasi ya 16 wakiwa na pointi 15.

Nani ataibuka mshindi? Yote hayo yatathibitishwa leo usiku.