Bordeaux tayari kumsajili Giroud ila nyota huyo ataka kuhamia Inter Milan

Bordeaux wanataka kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Olivier Giroud mwezi Januari, lakini mshambuliaji huyo wa Ufaransa anatumai kujiunga na Inter Milan. (Goal)

Msambuliaji wa zamani wa Manchester United na Sweden Zlatan Ibrahimovic, 38, yupo radhi kuhamia Everton pale Carlo Ancelotti atakapokabidhiwa rasmi klabu hiyo. (Talksport)

Mkufunzi wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer anasema kuwa klabu hiyo iko tayari kufanya kazi na Mino Raiola kumnasa mshambuliaji wa miaka 19-kutoka Norway Erling Haaland kutoka Red Bull Salzburg.(Sunday Mirror)

Raiola pia anamwakilisha kiungo wa kati wa United Paul Pogba, 26, na ameambiwa na Real Madrid kuwa hawataweka dau la kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwezi Januari. (Marca)