Msambuliaji wa zamani wa Manchester United na Sweden Zlatan Ibrahimovic, 38, yupo radhi kuhamia Everton pale Carlo Ancelotti atakapokabidhiwa rasmi klabu hiyo. (Talksport)
Mkufunzi wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer anasema kuwa klabu hiyo iko tayari kufanya kazi na Mino Raiola kumnasa mshambuliaji wa miaka 19-kutoka Norway Erling Haaland kutoka Red Bull Salzburg.(Sunday Mirror)
Raiola pia anamwakilisha kiungo wa kati wa United Paul Pogba, 26, na ameambiwa na Real Madrid kuwa hawataweka dau la kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwezi Januari. (Marca)
Spurs pia wanataka kumleta beki wa Ufaransa Issa Diop, 22, ambaye thamani yake inakadiriwa na West Ham United kuwa £50m .(Sky Sports)
Mshambuliaji wa Brescia and Italia Mario Balotelli anataka kubakia katika klabu hiyo ili mradi mmiliki wa klabu hiyo Massimo Cellino yuko makini kuendelea kumbakisha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29. (Football Italia)