- Doreen Majala awaambia wanamitandao waache tabia ya kuwashambuliwa waathiriwa wa ukatili wa kijinsia
Wakili na mwanahabari Doreen Majala amewaambia wanamitandao wakome kuwashambulia waathiriwa wa ukatili wa kijinsia ambao hujitokeza na kuzungumzia hali yao.
KUlingana na Majala watu kama hao hupitia mengi baada ya kujitambulisha wao ni akina nani na kwamba wana maisha yao baada ya shida yoyote.
Pia alisema kuwa amepitia hayo na kuwa mitandao ya kijamii inaweza kuvunja au kujenga mtu.
Wakili huyo alisema kwamba ukatili wa kijinsia umeongezeka sana.
"Kesi za ukatili wa kijinsia zinaongezeka. Leo nazungumza. Kama mtu ambaye alitembea njia hiyo. Vyombo vya habari vya kijamii ni jukwaa la ushawishi, linaweza kujenga / kuvunja
Wacha tuachane na aibu na kushambulia waathiriwa ambao hutoka nje. Mwanaume / Mwanamke
Hadi upate uzoefu au mpendwa, unaweza usiweze kuelewa ukubwa. Kwa wanablogu ambao ni wenzangu katika tasnia ya habari, unapowasilisha hadithi zaukatili wa kijinsia kumbuka kutunza hadhi ya waathiriwa
To bloggers who are my fellow colleagues in the media industry, as you highlight GBV stories, remember to uphold the dignity of victims. Let’s not publish headlines for views. Some victims withstand heat while others get a mental breakdown. Everyone has a life after any ordeal.
— Doreen Majala (@doreenmajala) April 23, 2021
Tusichapishe vichwa vya habari kwa maoni. Waathiriwa wengine huhimili joto wakati wengine hupata shida ya akili. Kila mtu ana maisha baada ya shida yoyote." Aliandika Majala.