logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Akothee alalamika mama aliyelipia rent siku 4 zilizopita kumpigia tena akitaka chakula

Katika hali ya kushangaza, Akothee Alifichua kwamba mwanamke huyo hata hakuweza kulipa kodi hiyo na kumtaja kama mama mwenye umri wa miambaye ni mvivu kupindukia.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani15 April 2025 - 08:08

Muhtasari


  • Hata hivyo, kilichompandisha mori Akothee ni baada ya mwanamke huyo kurudi kwake tena safari hii akiwa na hitaji jipya la kutaka msaada wa hela za kununua chakula.
  • Katika hali ya kushangaza, Akothee Alifichua kwamba mwanamke huyo hata hakuweza kulipa kodi hiyo na kumtaja kama mama mwenye umri wa miambaye ni mvivu kupindukia.

Akothee

MJASIRIAMALI Esther Akothee ameonyesha kughafilika kwake baada ya mwanamke mmoja aliyemsaidia takribani wiki moja iliyopita kurudi kwake tena akihitaji msaada zaidi.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Akothee alichapisha ujumbe huo akisema kwamba siku 4 zilizopita, mwanamke huyo alimlilia kwamba hakuwa na mahali pa kulala baada ya kufungiwa nyumba.

Alimlilia msanii huyo ambaye kwa utu aliguswa na kumlipia kodi ya kila mwezi ya shilingi elfu 6.

Hata hivyo, kilichompandisha mori Akothee ni baada ya mwanamke huyo kurudi kwake tena safari hii akiwa na hitaji jipya la kutaka msaada wa hela za kununua chakula.

Ni suala lililoonekana kumkera Akothee ambaye alilichapisha kwenye Facebook yake na kuvutia maoni mseto, baadhi wakihisi mwanamke huyo aliyesaidiwa alikwenda hatua zaidi ya kuwa na mazoea.

“Unakumbuka yule mama fua nilimtumia 6k siku 4 zilizopita kumlipia malimbikizo ya nyumba yake? Alipiga simu jana kuomba pesa tena akisema anahitaji msaada wangu na hana hata 50 bob kumudu mahali pa kulala. "Boss ni mimi petronila, tafadhali mum, Leo sina magali pa Kulala, nitumie kitu kidogo nijisaidie1" Akothee alisema.

Katika hali ya kushangaza, Akothee Alifichua kwamba mwanamke huyo hata hakuweza kulipa kodi hiyo na kumtaja kama mama mwenye umri wa miambaye ni mvivu kupindukia.

“Hajawahi kulipa kodi alisema mwenye nyumba hakuwahi kupokea simu zake 🙏Kwa hivyo niliachana na vita kwa sababu nimeshindwa, yeye ni mvivu hata kutunza kwa muda mrefu, anaficha nguo chafu na huwa na haraka ya kuondoka, hawezi kupika wala kusafisha nyumba vizuri, hadithi zake zote hazijumuishi yeye ni marehemu 50s 🙏 Mungu tafadhali, sitaki kuwa yeye nikua niache nibaki mitaani.  Na hii uwomgo wa ujinga haha ​​upate billionaire, huwezi kujenga punje inaishia hapo,” alisema.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved