Baba Talisha apoteza akaunti yake ya TikTok saa chache baada ya kufikisha wafuasi milioni 1

“Maisha yanaendelea tu” Baba Talisha alisema akithibitisha akaunti yake kufungwa, muda mfupi baada ya kusherehekea kufikisha wafuasi milioni 1.

Muhtasari

• Uwepo wake kwenye TikTok uliongezeka wakati rafiki yake, TikToker Brian Chira alikuwa akiishi naye.

• Wawili hao waliwatumbuiza wanamtandao kupitia vipindi vyao vya moja kwa moja huku pia wakipokea zawadi nyingi kutoka kwao.

BABA TALISHA na bintiye wajishindia likizo kwa hisani ya EXPEDITIONS MAASAI SAFARIS
BABA TALISHA na bintiye wajishindia likizo kwa hisani ya EXPEDITIONS MAASAI SAFARIS
Image: FACEBOOK

Faustine Lipuku Lukale, maarufu kama Baba Talisha katika mtandao wa TikTok amepatwa na pigo baada ya kupoteza akaunti yake ya TikTok.

Hii inajiri muda mchache baada ya kusherehekea kufikisha wafuasi milioni moja katika mtandao huo wa video fupi.

Akithibitisha taarifa hizo mbaya kupitia ukurasa wake wa instaram, Baba Talisha alipiga picha ya akaunti yake ya TikTok yenye wafuasi milioni moja ambapo ilionekana imeandikwa kwamba imepigwa marufuku.

“Maisha yanaendelea tu” Baba Talisha aliandika kwenye picha hiyo.

Kabla ya kupoteza akaunti hiyo, Baba Talisha alisherehekea kufikisha milioni moja ya wafuasi baada ya miezi kadhaa ya kuwa kwenye programu.

Pia alikuwa amefanikiwa kupata zaidi ya watu Milioni 42 waliopendezwa na video zake zote za TikTok. Kupitia ukurasa wake rasmi wa TikTok, wasifu ulionyesha kwa fahari nambari ya Milioni 1.0, kuthibitisha ushawishi wake kwenye programu.

Amekuwa akifanya matangazo mengi ya moja kwa moja akivuta umati mkubwa kwake.

Uwepo wake kwenye TikTok uliongezeka wakati rafiki yake, TikToker Brian Chira alikuwa akiishi naye. Wawili hao waliwatumbuiza wanamtandao kupitia vipindi vyao vya moja kwa moja huku pia wakipokea zawadi nyingi kutoka kwao.

Baadaye Chira alipoaga dunia, Baba Talisha aliwahamasisha Wakenya kuchangia mazishi yake. Watu wenye mioyo fadhili waliona zaidi ya Ksh. 8M ilipitia kwake ili kumpa Chira buriani ya maana.

Baba Talisha alipata sifa nyingi kutoka kwa Wanamtandao kwa kuchangisha kiasi hicho cha fedha na kusimama na bibi yake Chira katika kipindi kigumu zaidi. Kama matokeo ya fadhili zake, alizawadiwa likizo yenye malipo kamili na mashirika tofauti kama shukrani.