Rekodi ya awali ya mbio hizo ilikuwa ikishikiliwa na Paula Radcliffe kwa kipindi cha miaka 16 iliyopita.
Kosgei alijizatiti na akamaliza katika muda wa 2:14:04, zaidi ya dakika sita mbele ya Ababel Yeshaneh, ambaye alikimbia masaa mawili, dakika 20 na sekunde 51, na Gelete Burka ambaye alikimbia masaa mawili, dakika 20 na sekunde 55 wakati Ethiopia ilimaliza katika nafasi ya pili na tatu.
Mwanariadha huyu mwenye umri wa miaka 25 alishinda kwa mara ya kwanza katika mashindano ya London maratahon mapema mwaka huu, na sasa ameshinda kwa mara ya tatu baada ya ushindi huko Chicago mwaka 2018.
Kosgei alipongezwa na Radcliffe baada ya kunyakua taji hilo la bingwa wa dunia katika mbio za masafa marefu kwa kina dada.
Rekodi iliyovunjwa na Brigid Kosgei ilithibitishwa na shirika la IAAF kwa kuwa alikimbia katika madhari ya mashindano yaliyo rasmi kinyume na mbio za Kipchoge ambapo hapakuwa na mshindani na alisaidiwa na wanariadha wengine 41 kufanikisha mbio hizo.
Alimaliza wikendi ya kupendeza katika fani ya riadha Jumapili baada ya Eliud Kipchoge kutawazwa mwanariadha wa kwanza duniani kukimbia mbio za kilomita 42 chini ya saa mbili.