Wahadhiri 85 katika chuo cha teknologia cha Pwani wapinga vikali za serikali

KUPPET Secretary General Akello Missori
KUPPET Secretary General Akello Missori
Zaidi ya wahadhiri 85 katika chuo cha teknologia cha Pwani mjini Voi wamepinga vikali hatua ya serikali  ya kupunguza mishahara yao bila kutoa notisi.
 
Akizungumza chuoni humo mapema hii leo,katibu mkuu wa muungano wa KUPPET tawi la Taita Taveta Shedrack Mutungi amesema huendi jambo hilo limetokana na hatua ya serikali ya kuhamisha walimu hao kutoka kwa tume ya TSC hadi tume ya wafanyikazi wa umma(PSC).
 
Anasema hatua hiyo inakiuka agizo la mahakama linalozuia uhamisho wa walimu wa vyuo vya kadri (TVET) kote nchini hadi PSC na kuitaka serikali kuwalipa mishahara yao kikamilifu la sivyo wawasilishe kesi mahakamani.
 
Uhamisho huo umeathiri kiwango cha marupurupu yanayotolewa kwa walimu huku wengine wakikatwa kati ya shilingi elfu 12 na elfu 40.